jumaa, 07 Novemba 2014 09:23
Kushtadi uvamizi na hujuma za utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya
Masjid al-Aqswa ambazo katika siku za hivi karibuni zimechukua mkondo
hatari zaidi kuliko huko nyuma, kumekabiliwa na radiamali za makundi ya
Wapalestina katika uga wa kimuqawama na kisiasa. Katika mazingira kama
haya, sanjari na malalamiko ya wananchi dhidi ya utawala wa Kizayuni
unaoikalia kwa mabavu Quds Tukufu, makundi ya mapambano ya Palestina
yamebainisha kwamba, muqawama na mapambano ndilo chaguo pekee la kuuhami
na kuulinda msikiti wa al-Aqswa na uvamizi mtawalia wa utawala haramu
wa Israel. Katika uwanja huo, siku ya Jumatano Khalid Mash’al, Mkuu wa
Ofisi ya Kis
iasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS
alisisitiza kwamba, machaguo na mikakati yote ya kuuhami msikiti wa
al-Aqswa inazingatiwa, lakini muqawama ndilo chaguo linaloongoza
machaguo yote. Katika mazingira kama haya, balozi na mwakilishi wa
Palestina katika Umoja wa Mataifa, amelitaka Baraza la Usalama la Umoja
huo liushinikize utawala vamizi wa Israel ukomeshe vitendo vyake vya
utumiaji mabavu huko Baytul Maqaddas na katika Masjid al-Aqswa, kibla
cha kwanza cha Waislamu. Akizungumza na waandishi wa habari siku ya
Jumatano baada ya kikao cha faragha cha Baraza la Usalama la Umoja wa
Mataifa, Riyadh Mansour alisema, wanachama 15 wa baraza hilo wanapaswa
kuchukua msimamo wa kuitaka Israel ikomeshe harakati zozote zile za
siasa za kichochezi na vitendo vya utumiaji mabavu dhidi ya Wapalestina.
Mwakilishi huyo wa Palestina katika Umoja wa Mataifa ametangaza kuwa,
hatua ya Wazayuni wenye kufurutu ada wanaoingia na viatu katika msikiti
wa al-Aqswa ni ya kichochezi na imekuwa ikipelekea kutokea rangaito,
vurugu na mapigano. Ombi la Wapalestina kwa Baraza la Usalama la Umoja
wa Mataifa la kuitaka asasi hiyo iingilie kati kuhusiana na uvamizi na
vitendo vya kuuvunjia heshima msikiti wa al-Aqswa vinavyofanywa na
Wazayuni linatolewa katika hali ambayo, vitendo vya kuyavunjia heshima
matukufu ya Kiislamu vinavyofanywa na utawala huo vimeshadidi mno katika
eneo hilo takatifu, kongwe na la kihistoria, hali ambayo imepelekea
mgogoro wa Palestina kuingia katika marhala hatari zaidi. Hapana shaka
kuwa, hujuma na hatua za utawala vamizi wa Israel zimehatarisha amani na
usalama wa kimataifa. Hii ni katika hali ambayo, Baraza la Usalama la
Umoja wa Mataifa ambalo lina jukumu la kushughulikia masuala kama haya
limeamua kukaa kimya na kutochukua hatua yoyote ile ya maana. Hatua za
utawala ghasibu wa Israel katika msikiti wa al-Aqswa mbali na kukabiliwa
na malalamiko ya wananchi zimeandamwa pia na upinzani wa Waislamu
katika pembe mbalimbali ulimwenguni. Katika anga kama hii, fikra za
waliowengi ulimwenguni nazo zinafuatilia kwa hisia na unyeti maalumu
duru mpya ya hujuma za Wazayuni dhidi ya msikiti wa al-Aqswa na zinataka
Baraza la Usalama lichukue hatua za maana dhidi ya utawala huo. Katika
mazingira kama haya, Wapalestina wanataka kuchunguzwa haraka vitendo vya
utawala bandia wa Israel katika Masjid al-Aqswa na kuchukuliwa hatua za
maana na madhubuti za kusitisha hujuma za utawala huo ghasibu. Hii ni
katika hali ambayo, ripoti zinaonesha kuwa, Marekani inapinga vikali
kuzungumziwa suala la uvamizi wa Israel katika Masjid al-Aqswa kwenye
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa. Jambo lililo wazi ni kuwa, katika
hali ambayo utawala wa Kizayuni wa Israel unaendelea na hatua na hujuma
zake huko Quds katika anga ya kimya cha jumuiya za kimataifa, hatua
bora, ya maana na yenye taathira ni kuendelezwa muqawama sambamba na
kushadidishwa mapambano ya wananchi dhidi ya utawala huo ghasibu; na huu
ndio ukweli ambao umeashiriwa na Khalid Mash’al, Mkuu wa Ofisi ya
Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS. Matukio
ya Palestina yanaonesha juu ya kuingia Wapalestina katika marhala mpya
ya muqawama na mapambano dhidi ya utawala vamizi wa Israel. Katika
mazingira kama haya, wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanaamini kwamba,
uvamizi na hujuma za Israel dhidi ya msikiti wa al-Aqswa ni kitendo cha
kuwasha moto ambao utawala huo ghasibu utatumbukia wenyewe
0 toamaon yako: