Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Friday, November 7

Ban atakiwa kufuatilia jinai za utawala wa Bahrain

Posted by mkachu  |  Tagged as:

Ban atakiwa kufuatilia jinai za utawala wa BahrainChama cha upinzani cha al Wefaq nchini Bahrain kimemtaka Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon afuatilie jinai za utawala wa al Khalifa.  Sheikh Ali Salman, Katibu Mkuu wa chama hicho amesema, kukamatwa tena Nabil al Rajab na viongozi wengine wa upinzani wa Bahrain na kupigwa marufuku shughuli za chama cha la Wefaq ni sawa na kushindwa uchaguzi wa Bunge la nchi hiyo hata kabla ya kufanyika. Katika barua yake kwa Ban Ki-moon ameeleza kuwa, vikosi vya utawala wa Bahrain vinawatesa hadi kufa wapinzani huku kuvunjwa haki za binadamu na kukandamizwa watu likiwa ni jambo la kawaida nchini humo. Ameongeza kwamba, utawala wa Aal Khalifa mbali na kubomoa misikiti, umeshadidisha sera za ubaguzi wa kidini na kutumia gesi za sumu dhidi ya waombolezaji wa Imam Hussein (A.S).
Katibu Mkuu wa chama cha upinzani cha la Wefaq sambamba na kusisitiza kuendelea harakati za kimapinduzi za wananchi amemtaka Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ashughulikie jinai zinazofanywa na utawala wa Manama.

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com