Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Friday, November 21

Rais wa Somalia: al-Shabab watasambaratishwa

Posted by mkachu  |  Tagged as:

Rais wa Somalia: al-Shabab watasambaratishwaRais Hassan Sheikh Mohamoud wa Somalia ametangaza kuwa, hadi kufikia mwishoni mwa mwaka huu wa 2014, kundi la wanamgambo wa al-Shabab litalazimika kuondoka katika maeneo na miji linayoidhibiti katika nchi hiyo ya Pembe ya Afrika. Mtandano wa Habari wa al-Yaum Sab’i umemnukuu Rais Hassan Sheikh Mohamoud akisema kwamba, hadi kufikia mwishoni mwa mwezi Desemba ujao jeshi la Somalia na vikosi vya kusimama amani vya Umoja wa Afrika AMISOM vitakuwa vimefanikiwa kuwafurusha wanamgambo wa al-Shabab na kuwalazimisha kuondoka katika maeneo wanayoyadhibiti.
 Rais wa Somalia ambaye kwa sasa yuko nchini Denmark alikokwenda kushiriki mkutano wa kimataifa kuhusu Somalia amesema kuwa, wanamgambo wa al-Shabab watalazimika kurejea nyuma na kwenda katika vijiji vya mbali na hivyo mashambulio yao baada ya hapo yatakuwa ya hapa na pale. Rais Mohamoud amebainisha kwamba, serikali ya Somalia inafanya kila iwezalo ili kuhakikisha kwamba, hadi kufikia miezi mitatu ya awali ya mwaka ujao wa 2015 kusiweko  eneo lolote nchini humo ambalo linadhibitiwa na wanamgambo wa al-Shabab.

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com