Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Sunday, October 12

UN:Ebola kudhibitiwa kwa miezi mitatu

Posted by mkachu  |  Tagged as:

Mjumbe wa Umoja wa Mataifa anayehusika na ugonjwa wa Ebola David Nabarro ameiambia BBC kuwa mlipuko wa ugonjwa huo magharibi mwa Afrika unaweza kudhibitiwa katika kipindi cha miezi mitatu.
Dr.Nabarro alisema kuwa ina maana kuwa visa vipya vya ugonjwa huo vitapungua kila wiki.
Amesema kuwa kwa sasa maambukizi ya ugonjwa wa Ebola ni ya juu hata baada ya kuwepo kwa jitihada za kimataifa.
Nabarro amesema kuwa kuuelewa ugonjwa wa Ebola miongoni mwa jamii zilizoathirika kutasaidia kupambana nao kwa kuwa watu wanaelewa kwamba kuwatenga wagonjwa ndiyo njia bora ya kuzuia maambukizi.
Zaidi ya watu 4000 wameaga dunia kutokana na ugonjwa wa Ebola wengi kutoka mataifa ya Sierra Leone, Liberia na Guinea.

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com