Wafadhili wamekusanyika mjini Cairo, Misri ili kujadili misaada
inayohitajika kwa ajili ya kukarabati Ukanda wa Gaza ulioharibiwa katika
mashambulizi ya hivi karibuni kati ya utawala wa Kizayuni wa Israel.
Mamlaka ya Ndani ya Palestina imesema kuwa dola bilioni 4 zinahitajika kwa ajili ya kujenga tena Ukanda wa Gaza. Wapalestina wasiopungua 100,000 huko Gaza wamebaki bila makazi kutokana na uharibufu mkubwa uliofanywa na jeshi la Israel, huku miundo mbinu ya eneo hilo ikiharibiwa vibaya.
Wakati huo huo Mkuu wa Kamati ya Wananchi ya Kukabiliana na Mzingiro wa Gaza amesema kuwa, mkutano wa kukarabati Gaza ni fursa kwa ajili ya kuondoa mzingiro wa kidhulma kwenye eneo hilo. Jamal al Khadhwari amesisitiza kuwa, mkutano wa kimataifa unaofanyika Cairo ni fursa nzuri kwa ajili ya kuchukuliwa misimamo ya kimataifa ya kuilazimisha Israel iondoe mzingiro wa miaka 8 dhidi ya Ukanda wa Gaza.
Mamlaka ya Ndani ya Palestina imesema kuwa dola bilioni 4 zinahitajika kwa ajili ya kujenga tena Ukanda wa Gaza. Wapalestina wasiopungua 100,000 huko Gaza wamebaki bila makazi kutokana na uharibufu mkubwa uliofanywa na jeshi la Israel, huku miundo mbinu ya eneo hilo ikiharibiwa vibaya.
Wakati huo huo Mkuu wa Kamati ya Wananchi ya Kukabiliana na Mzingiro wa Gaza amesema kuwa, mkutano wa kukarabati Gaza ni fursa kwa ajili ya kuondoa mzingiro wa kidhulma kwenye eneo hilo. Jamal al Khadhwari amesisitiza kuwa, mkutano wa kimataifa unaofanyika Cairo ni fursa nzuri kwa ajili ya kuchukuliwa misimamo ya kimataifa ya kuilazimisha Israel iondoe mzingiro wa miaka 8 dhidi ya Ukanda wa Gaza.
0 toamaon yako: