Leo ni Jumapili tarehe 17 Mfunguo Tatu Dhul-Hijja mwaka 1435 Hijiria, inayosadifiana na tarehe 12 Oktoba mwaka 2014 Miladia.
Siku
kama ya leo miaka 482 iliyopita wakoloni wa Kihispania walianzisha
mashambulizi chini ya uongozi wa Francois Pizarro dhidi ya ardhi
inayojulikana hii leo kwa jina la Peru. Wakati huo kaumu ya Inka ambayo
ni moja kati ya kaumu za America ya Latini ndiyo iliyokuwa ikitawala
eneo hilo. Viongozi wa kaumu hiyo hawakutilia maanani uvamizi wa
Wahispania huku wakisalia bila kuchukua hatua zozote za kukabiliana na
wavamizi hao. Baada ya kudhibitiwa ardhi ya Peru na wavamizi hao,
Pizarro alimtaka mtawala wa Inka kuwa chini ya himaya ya Uhispania
lakini akakataa pendekezo hilo. Pizarro alitoa amri ya mauaji ya umati
dhidi ya watu wa kaumu hiyo mauaji yanayohesabiwa kuwa makubwa na mabaya
zaidi katika historia ya America ya Latini. Ukubwa wa mauaji hayo ndio
uliopelekea kuporomoka ustaarabu na utawala wa miaka mingi wa Inka.
Siku
kama ya leo miaka 46 iliyopita, Guinea ya Ikweta (Equa
torial Guinea)
ilifanikiwa kupata uhuru wake kutoka kwa mkoloni Muhispania, na siku hii
hutambuliwa kama siku ya kitaifa nchini humo. Equatorial Guinea
iligunduliwa na mabaharia wa Ureno katika karne ya 15 Miladia. Ureno
ulikikabidhi kisiwa hicho kwa Uhispania hapo mwaka 1778 Miladia, huku
ukoloni wa Wahispania dhidi ya Equatorial Guinea ukiendelea hadi mwaka
1968 ambapo nchi hiyo ilijipatia uhuru wake. Equatorial Guinea inapakana
na nchi za Gabon na Cameroon.
Siku kama ya leo miaka 15 iliyopita,
Jenerali Parviz Musharraf, mkuu wa majeshi ya Pakistan alifanya
mapinduzi yasiyo ya umwagaji damu na kumuondoa madarakani Muhammad Nawaz
Sharrif Waziri Mkuu wa Pakistan wa wakati huo. Baada ya mapinduzi hayo
Musharraf ambaye alichukuwa wadhifa wa urais wa nchi hiyo, alivifanyia
mabadiliko baadhi ya vipengee vya katiba ya nchi hiyo, na kuongeza nguvu
za rais wa nchi. Lakini kutokana na kuongezeka mashinikizo ya ndani na
nje, Musharraf alisalimu amri mwezi Novemba 2007 na kuamua kung'atuka
kwenye wadhifa huo. Hata hivyo ilipofika mwezi Julai 2008, aliondoka
kikamilifu madarakani ikiwa ni baada ya kushika kasi vyama vya upinzani
na kushinda uchaguzi wa rais.
Leo ni tarehe 20 mwezi wa Mehri kwa
mujibu wa kalenda ya Kiirani, ambayo inasadifiana na maadhimisho ya
Khoja Shamsuddin Muhammad Hafez Shirazi, mshairi na malenga mkubwa wa
Kiirani. Hafez alizaliwa mwaka 727 Hijiria Shamsia, mjini Shiraz moja ya
miji ya kusini mwa Iran. Alikuwa mtaalamu katika Tafsiri ya Qur'an,
falsafa na fasihi ya Kiarabu huku akiwa mashuhuri kwa jina la Hafez
kutokana na kuhifadhi kwake Qur'an Tukufu kwa visomo tofauti. Mbali na
elimu hizo, Khoja Shamsuddin Muhammad Hafez, alikuwa mtaalamu mkubwa wa
elimu ya Irfan.
Sunday, October 12
Jumapili, Oktoba 12, 2014
Posted by mkachu |  Tagged as: leo katka hisory
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Andika Maoni
add
TANGAZANASI
kwama Matangazo wasiliana nasi kupitia anuani zifuataz
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
ZILIZO SOMWA ZAIDI
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa ni dua za baada ya nyakati mbalimbali za sala. Tunamuomba Mwenyezi Mung...
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa chini ni dua 25 za Qur'ani Tukufu tulizozinukuu kutoka katika...
-
RATIBA YA VIPINDI KWA JUMA ZIMA RATIBA - JUMATATU MUDA KIPINDI MUHUSIKA 06:30-07:00 M...
-
Rais Bashar al-Assad wa Syria amesema kuwa, kuna udharura wa kuweko vita vya kimataifa dhidi ya magaidi. Rais Assad amesisitiza kwamba, kwa...
MITANDAO YA KIJAMII
TAFUTA HABARI ZILIZO SOMWA NYUMA
Powered by Blogger.
Author
CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...
0 toamaon yako: