Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Thursday, October 2

Alkhamisi, 02 Oktoba, 2014

Posted by mkachu  |  Tagged as:

Alkhamisi, 02 Oktoba, 2014Leo ni Alkhamisi tarehe 7 Dhulhaji 1435 Hijria sawa na Oktoba 2, 2014.
Tarehe 7 Dhulhija miaka 1321 iliyopita, aliuawa shahidi Imam Muhammad Baqir AS mjukuu mtukufu wa Mtume wa Uislamu Muhammad (SAW) na mmoja wa Maimamu watoharibu katika kizazi chake. Imam Baqir AS alizaliwa katika mji mtakatifu wa Madina na kupata umashuhuri katika uwanja wa elimu, ambapo alikuwa akijibu maswali na masuala magumu ya zama na kwa sababu hiyo alipewa lakabu ya "Baqir" yaani mchimbua elimu. Kipindi cha uimamu wa mtukufu huyo kiliambatana na kudhoofika kwa utawala wa Bani Umayyah, suala ambalo lilimpa fursa nzuri ya kulea Waislamu wa zama hizo kifikra na kielimu. Imam Baqir (as) alisifika kwa ukarimu, kuwasamehe waliomkosea, kuwasaidia masikini na kuwatembelea wagonjwa. Redio Tehran inatoa mkono wa pole kwa Waislamu wote kwa mnasaba huu mchungu wa kuuliwa shahidi Imam Baqir (AS).
Siku kama ya leo miaka 827 iliyopita mwafaka na tarehe 2 Oktoba 1187, Swalahuddin Ayyubi kamanda wa jeshi la Kiislamu alifanikiwa kuikomboa Baitul Muqaddas katika Vita vya Msalaba. Baitul Muqaddas, ni kibla cha kwanza cha Waislamu na mahala ambako Mtume Mtukufu Muhammad SAW alianzia safari yake ya 'Miiraji' kuelekea mbinguni. Awamu ya kwanza ya Vita vya Msalaba ilianza mwaka 1095 Miladia na vilimalizika kabisa mwaka 1270 baada ya kushindwa kikamilifu jeshi la Msalaba.
Siku kama ya leo miaka 110 iliyopita sawa na tarehe Pili Oktoba 1904, alizaliwa mwandishi wa Uingereza Graham Greene. Vitabu vya msomi huyo viliakisi mpambano baina ya mema na mabaya na aliandika kwenye kitabu chake kinachoitwa 'Nguvu na Utukufu' kwamba subira, uvumilivu na mateso ni njia ya wokovu. Graham Greene ameacha vitabu vingi kama 'Mtu wa Tatu', 'Utawala wa Hofu' na 'Muuaji wa Kukodishwa'. Mwandishi huyo Muingereza alifariki dunia mwaka 1991.
Na siku kama ya leo miaka 73 iliyopita sawa na tarehe Pili Oktoba 1941, kiongozi wa Ujerumani ya Kinazi Adolph Hitler, alitoa amri ya kuanza awamu ya pili ya mashambulizi ya jeshi la hiyo dhidi ya Urusi ya zamani. Kwenye awamu ya kwanza ya mashambulizi ya jeshi la nchi hilo iliyoanza tarehe 22 Juni 1941, Ujerumani iliweza kuikalia kwa mabavu sehemu ya ardhi ya Urusi. Lengo la kufanywa shambulio hilo la dikteta Hitler, lilikuwa ni kurahisisha operesheni za kijeshi, kudhoofisha nguvu za Jeshi Jekundu na kudhibiti ardhi zaidi za Urusi hasa Moscow mji mkuu wa nchi hiyo.

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com