Rais
wa Afghanistan Ashraf Ghani anaongoza kikao maalum cha usalama baada ya
mashambulizi
kadha ya kujitolea muhanga yaliyopelekea watu 41 kufa.
Mji mkuu wa Afghanistan, Kabul, umekumbwa na milipuko kadhaa
Miongoni mwa maeneo yaliyolengwa ni chuo cha maafisa wa polisi, ambapo mtu mmoja aliyekuwa amevalia sare za polisi alijilipua na kuwaua zaidi ya watu 25.
Washambuliaji hao pia walivamia kituo cha wanajeshi wa shirika la kujihami la NATO kilichoko karibu na uwanja wa ndege wa kimataifa.

Inadaiwa kuwa wawili kati ya washambuliaji hao waliuawa.
Mapema siku ya Ijumaa lori moja lililokuwa limetegwa bomu lililipuka karibu na afisi za serikali na kuwaua watu 15.

Rais Ashraf Khan alisema kuwa mashambulizi hayo yalikuwa ni lengo la Wapiganaji wa Kiislamu wa Taliban kujaribu kuwasahaulisha watu misukosuko inayokumba kundi lao kufuatia tangazo la juma lililopita kuwa mwanzilisi wa kundi hilo,Mullah Omar,alifariki
0 toamaon yako: