Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Friday, November 21

Wakimbizi wa Chad wanakabiliwa na hali mbaya

Posted by mkachu  |  Tagged as:

Wakimbizi wa Chad wanakabiliwa na hali mbayaShirika la Kimataifa la Msalaba Mwekundu limeelezea wasi wasi wake mkubwa lilionao kuhusiana na hali mbaya wanayokabiliwa nayo wakimbizi wa Chad. Taarifa zaidi zinasema kuwa, baada ya kushadidi machafuko katika Jamhuri ya Afrika ya Kati, raia wengi wa Chad waliokuwa wakiishi nchini humo wamelazimika kuondoka nchini humo na kurejea 

nchini kwao. Aghlabu ya wakimbizi hao wamo katika kambi za wakimbizi zilizoko kusini magharibi mwa Chad. Kwa mujibu wa Shirika la Kimataifa la Msalaba Mwekundu hali ya kibinadamu katika kambi hizo ni mbaya mno. Takribani raia elfu saba kati ya wakimbizi hao wana azma ya kurejea katika makazi yao huko mashariki mwa Chad. Ripoti ya 

Shirika la Kimataifa la Msalaba Mwekundu inaeleza kuwa, licha ya kuweko ugawaji misaada kwa wakimbizi hao, lakini misaada hiyo haitoshi kukidhi mahitaji ya wakimbizi hao. Mbali na wakimbizi wa Kichadi waliorejea katika nchi yao, 


Chad kwa sasa inakabiliwa pia na wimbi la wakimbizi kutoka Jamhuri ya Afrika ya Kati ambao wameikimbia nchi yao baada ya kushadidi machafuko na mapigano. Umoja wa Mataifa umetangaza kwamba serikali ya Chad haina uwezo wa kifedha wa kudhamini mahitajio ya maelfu ya wakimbizi wa Jamhuri ya Afrika ya Kati walioko nchini humo.

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com