Shirika la Kimataifa la Msalaba Mwekundu limeelezea wasi wasi wake mkubwa lilionao kuhusiana na hali mbaya wanayokabiliwa nayo wakimbizi wa Chad. Taarifa zaidi zinasema kuwa, baada ya kushadidi machafuko katika Jamhuri ya Afrika ya Kati, raia wengi wa Chad waliokuwa wakiishi nchini humo wamelazimika kuondoka nchini humo na kurejea
nchini kwao. Aghlabu ya wakimbizi hao wamo katika kambi za wakimbizi zilizoko kusini magharibi mwa Chad. Kwa mujibu wa Shirika la Kimataifa la Msalaba Mwekundu hali ya kibinadamu katika kambi hizo ni mbaya mno. Takribani raia elfu saba kati ya wakimbizi hao wana azma ya kurejea katika makazi yao huko mashariki mwa Chad. Ripoti ya
Shirika la Kimataifa la Msalaba Mwekundu inaeleza kuwa, licha ya kuweko ugawaji misaada kwa wakimbizi hao, lakini misaada hiyo haitoshi kukidhi mahitaji ya wakimbizi hao. Mbali na wakimbizi wa Kichadi waliorejea katika nchi yao,
Chad kwa sasa inakabiliwa pia na wimbi la wakimbizi kutoka Jamhuri ya Afrika ya Kati ambao wameikimbia nchi yao baada ya kushadidi machafuko na mapigano. Umoja wa Mataifa umetangaza kwamba serikali ya Chad haina uwezo wa kifedha wa kudhamini mahitajio ya maelfu ya wakimbizi wa Jamhuri ya Afrika ya Kati walioko nchini humo.
IQRA FM RADIO
Friday, November 21
Wakimbizi wa Chad wanakabiliwa na hali mbaya
Posted by mkachu | Tagged as: Habari za kitaifa na kimataifa
Related Posts:
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Andika Maoni
add
LEO KATIKA HISTORIA
TANGAZANASI
kwama Matangazo wasiliana nasi kupitia anuani zifuataz
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
ZILIZO SOMWA ZAIDI
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa ni dua za baada ya nyakati mbalimbali za sala. Tunamuomba Mwenyezi Mung...
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa chini ni dua 25 za Qur'ani Tukufu tulizozinukuu kutoka katika...
-
RATIBA YA VIPINDI KWA JUMA ZIMA RATIBA - JUMATATU MUDA KIPINDI MUHUSIKA 06:30-07:00 M...
-
Sura ya Al Furqan, aya ya 41-44 (Darsa ya 628) Wasikilizaji wapenzi wa Darsa ya Qur'ani, Assalamu Alaykum Warahmatullahi Wa...
MITANDAO YA KIJAMII
TAFUTA HABARI ZILIZO SOMWA NYUMA
Powered by Blogger.
Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...
0 toamaon yako: