
Hayo yanajiri huku shirika la misaada la Hilali Nyekundu likiwaondosha wagonjwa katika hospitali kuu ya wazazi ya mji wa Benghazi baada ya mapigano kukaribia. Jeshi la Libya likisaidiwa na askari watiifu kwa jenerali mstaafu Khalifa Haftar linafanya operesheni ya kijeshi dhidi ya wanamgambo waliokuwa wakiudhibiti mji huo.
Zaidi ya watu 200 wameuawa mjini humo tangu jeshi lilipoanza operesheni za kuudhibiti mji huo kutoka kwa wanamgambo mwezi uliopita.
0 toamaon yako: