Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Monday, November 3

Wakazi wa Benghazi Libya watakiwa kuondoka

Posted by mkachu  |  Tagged as:

Wakazi wa Benghazi Libya watakiwa kuondokaJeshi la Libya limewataka raia wa wilaya ya kati ya mji wa Benghazi kuondoka katika makazi yao ili kupisha operesheni inayofanywa na vikosi vya jeshi dhidi ya wanamgambo kwenye mji huo. Ahmed al Mesmari msemaji wa vikosi vya jeshi la Libya amesema kuwa, wakazi wote wa wilaya ya Assabri wanatakiwa kundoka eneo hilo leo Jumatatu.
Hayo yanajiri huku shirika la misaada la Hilali Nyekundu likiwaondosha wagonjwa katika hospitali kuu ya wazazi ya mji wa Benghazi baada ya mapigano kukaribia.  Jeshi la Libya likisaidiwa na askari watiifu kwa jenerali mstaafu Khalifa Haftar linafanya operesheni ya kijeshi dhidi ya wanamgambo waliokuwa wakiudhibiti mji huo.
Zaidi ya watu 200 wameuawa mjini humo tangu jeshi lilipoanza operesheni za kuudhibiti mji huo kutoka kwa wanamgambo mwezi uliopita.

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com