Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Monday, November 3

EU yakosoa ugomvi wa madaraka nchini Somalia

Posted by mkachu  |  Tagged as:

EU yakosoa ugomvi wa madaraka  nchini SomaliaUmoja wa Ulaya (EU) umesema kuwa ugomvi wa kuwania madaraka nchini Somali unatishia kuimarishwa amani nchini humo. Alexander Rondos mwakilishi maalumu wa Umoja wa Ulaya katika eneo la Pembe ya Afrika leo ameelezea wasiwasi wake mkubwa kutokana na hitilafu kati ya Rais Hassan Sheikh Mahmoud wa Somali na  Waziri Mkuu wa nchi hiyo Abdiweli Shekh Ahmed. Amesema kuwa hitilafu kati ya viongozi hao zinatishia jitihada zinazofanywa kwa lengo la kuimarisha amani na utulivu nchini Somalia. Ameongeza kuwa Somalia inahitajia amani na kwamba ugomvi wao wa madaraka tayari umeshaathiri utendaji wa taasisi za nchi hiyo na serikali kwa ujumla.
Waziri Mkuu wa Somalia mwezi uliopita alifanyia mabadiliko Baraza lake la Mawaziri na kuwaondoa mawaziri kadhaa mbao wapo karibu na rais wa nchi hiyo. Mabadiliko hayo yamepelekea viongozi wawili hao waingie katika mzozo na mvutano mkubwa wa kisiasa.

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com