Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Monday, November 3

Mashia ulimwenguni waomboleza siku ya Tasua

Posted by mkachu  |  Tagged as:

Mashia ulimwenguni waomboleza siku ya Tasua
Mamilioni ya wapenzi na wafuasi wa Imam Hussein bin Ali (A.S) nchini Iran na sehemu mbalimbali duniani wameshiriki katika maombolezo ya Tasua, siku ya 9 ya masaibu yaliyompata  mjukuu huyo wa Bwana Mtume SAW na wafuasi wake katika jangwa la Karbala huko Iraq ya leo.  Maombolezo ya Tasua hufanyika siku moja kabla ya siku ya Ashura, ambayo Imam Hussein (A.S) aliuawa kikatili na jeshi la Yazid bin Muawiyyah katika mapambano yake ya kulinda dini ya Mwenyezi Mungu. Hii ni katika ha li ambayo mamilioni ya Waislamu wa madhehebu ya Shia kutoka maeneo mbalimbali duniani wamekusanyika katika mji mtukufu wa Karbala iliopo Haram tukufu ya Imam Hussein AS, kwa ajili ya maadhimisho ya Tasua na Ashura.
Mbali na Iran na Iraq maombolezo ya Tasua pia yamefanyika kwa wingi katika nchi za Pakistan, Jamhuri ya Azerbaijan na Lebanon huku hafla kama hizo pia zikifanywa na waumuni wa madhehebu ya Kiislamu ya Shia duniani kote.

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com