Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Friday, November 7

UN yakosolewa kushindwa kuwalinda raia CAR

Posted by mkachu  |  Tagged as:

UN yakosolewa kushindwa kuwalinda raia CARShirika la Msamaha Duniani la Amnesty International limeukosoa Umoja wa Mataifa kwa kushindwa kulinda raia katika Jamhuri ya Afrika ya Kati, huku machafuko yakiendelea nchini humo. Amnesty imesema licha ya kuwepo mpango mpya wa UN katika nchi hiyo, lakini makumi ya raia wakiwemo watoto wameuawa na maelfu ya wengine kuhama makazi yao katika wiki za hivi karibuni. Shirika hilo la kutetea haki za binadamu pia limekitaka kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Mataifa kilichopo Jamhuri ya Afrika ya Kati kuchukua hatua madhubuti za kuwalinda raia katika wimbi jipya la mashambulio yanayowalenga Waislamu nchini humo.
 Ripoti zinasema kuwa zaidi ya watu 5,000 wameuawa katika nchi hiyo ya katikati mwa Afrika tangu Disemba mwaka jana, nchi hiyo ilipotumbukia kwenye machafuko. Machafuko hayo yalianza baada ya genge la Kikristo la Anti Balaka kuanza kuwashambulia Waislamu. 

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com