
Katika upande mwingine Iraq imesema
kuwa, kikosi chake cha anga kimeshambulia maeneo kadhaa ya magaidi wa
Daesh katika mikoa ya Salahuddin na Anbar kaskazini mwa mji mkuu
Baghdad. Hayo yanajiri huku jeshi la Iraq likifanikiwa kukomboa vijiji
kadhaa vilivyokuwa vimetekwa na waasi wa Daesh huku mapigano yakiendelea
ili kuzuia magaidi hao wasidhibiti mji wenye utajiri wa mafuta wa
Baiji.
Siku ya Jumatatu Waziri Mkuu wa Iraq
Haidar al Abadi alisema kuwa, mafanikio ya jeshi la nchi hiyo
yaliyopatikana hivi karibuni dhidi ya kundi la kitakfiri la Daesh
hayakusaidiwa na mashambulizi ya anga ya Marekani.
0 toamaon yako: