Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Friday, November 7

NAM yalaani kushambuliwa Wapalestina na Israel

Posted by mkachu  |  Tagged as:

NAM yalaani kushambuliwa Wapalestina na IsraelJumuiya ya Nchi Zisizofungamana na Siasa za Upande Wowote (NAM) imelaani mashambulio ya hivi karibuni ya Israel dhidi ya wananchi madhlumu wa Palestina. Ghulam-Hussein Dehqani, mwakilishi wa Iran katika Jumuiya hiyo amesema kwamba, mashambulio ya kila siku, kubomolewa nyumba na miundombinu katika Ukanda wa Gaza na kushambuliwa vituo vya umeme, hospitali na vyanzo vya maji na pia maeneo ya Umoja wa Mataifa sio tu ni janga kubwa bali ni ukiukwaji wa wazi wa haki za binadamu. Ameongeza kuwa, Israel pia inakiuka haki za raia wa Palestina na hasa huko Quds Mashariki na kutaka utawala huo ghasibu uchukuliwe hatua kimataifa.
 Katika upande mwingine Mussa Abu Marzuq mjumbe wa ofisi ya kisiasa ya harakati ya Hamas ametahadharisha juu ya kukaririwa njama za kuugawa msikiti mtukufu wa al Aqswa. Amesema kuwa, Israel inataka kuugawa msikiti mtukufu wa al Aqswa kati yake na Palestina kama ulivyofanya katika msikiti wa Nabii Ibrahim (A.S). Ameongeza kuwa Wapalestina na Waislamu duniani watachukua hatua dhidi ya njama za kuugawa msikiti huo na Israel haipaswi kusahau matukio ya hivi k aribuni yaliyojiri katika mji wa Quds.

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com