Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Friday, November 7

Kesi za Ebola zaongezeka nchini Sierra Leone

Posted by mkachu  |  Tagged as:

Kesi za Ebola zaongezeka nchini Sierra LeoneUmoja wa Mataifa umetangaza kuwa kesi za maambukizi ya ugonjwa wa Ebola zimeongezeka nchini Sierra Leone huku nchi hiyo ikikabiliwa na tatizo la ukosefu wa vituo vya matibabu. Mpango wa Dharura wa Kukabiliana na Ebola wa Umoja wa Mataifa (UNMEER) umesema wiki hii kuwa, mfumuko wa ugonjwa wa Ebola umesababisha vifo vya watu zaidi ya 1,060 nchini Sierra Leone huku maeneo yaliyoathiriwa zaidi yakiwa ya magharibi mwa mji mkuu Freetown.  Mpango huo aidha umesema, ukosefu wa vitanda katika vituo vya kutibu Ebola umesababisha familia kuangalia zenyewe wagonjwa majumbani, ambako waangalizi huwa hawana uwezo wa kutosha wa kujilinda wasiambukizwe virusi vya ugonjwa huo, na kwa sababu hiyo maambukizo yameongezeka.
Jumatano Shirika la Afya Duniani (WHO) liliripoti kuwa, idadi ya kesi za maambukizo ya Ebola zinaongezaka nchini Sierra Leone, ingawa ugonjwa huo umepungua katika nchi ya Liberia huku nchini Guinea maambukizo yakiwa ya wastani.

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com