Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Wednesday, October 8

Watu 9 wauawa katika maandamano Uturuki

Posted by mkachu  |  Tagged as:

 Watu 9 wauawa katika maandamano UturukiWatu wasiopungua 9 wameuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa katika maandamano yaliyoshuhudiwa katika miji kadhaa nchini Uturuki. Maandamano hayo yamefanywa na jamii ya Wakurdi kulalamikia kutochukua hatua serikali ya Ankara kuwasaidia Wakurdi waliovamiwa na magaidi wa Daesh katika mji wa Kubani ulioko kwenye mpaka wa nchi hiyo na Syria.  Gavana wa mji wa Istanbul amesema, miji ya Ankara na Istanbul pia ilishuhudia maandamano na ghasia ambapo zaidi ya watu 30 wamejeruhiwa wakiwemo polisi 8.  Wakati huo huo miji 6 ya mashariki mwa Uturuki imewekewa sheria ya kutotoka nje kuhofia uwezekano wa kushambuliwa kutoka upande wa mpaka wa Syria. Jumatatu Waziri Mkuu wa Uturuki Ahmet Davutoglu alisema kuwa, wako tayari kufanyakila wawezalo kuhakikisha kuwa mipaka ya nchi hiyo inalindwa dhidi ya mashambulizi ya kundi la Daesh.

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com