Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Wednesday, October 8

Waislamu wa Kisuni nchini Iran walaani jinai za Daesh

Posted by mkachu  |  Tagged as:

Muhammad Qasim Uthmani, Mbunge wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu
Mbunge Msuni katika Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema kuwa, Waislamu wa Kisuni nchini Iran wanalichukia kundi la kigaidi la Daesh. Bw. Muhammad Qasim Uthmani, mmoja wa wabunge hao amesema leo katika kikao cha wazi cha Bunge la Iran kwamba Masuni wa Iran wanalaani vikali jinai za kundi la kigaidi na kibaath la Daesh nchini Iraq na Syria na kuongeza kuwa, baada ya j inai zilizofanyika huko Ghaza Palestina na Shangal nchini Iraq, sasa ni wakati wa kufanyika jinai katika eneo la Kobani huko Syria. Mbunge huyo wa Iran ameongeza kuwa, mji wa Kobani na wananchi wasio na ulinzi wa mji huo wananyanyaswa na kuuliwa kinyama hivi sasa na kundi lenye fikra potofu la Daesh. Bw. Uthmani ameongeza kuwa, inasikitisha kuona kuwa, kama ilivyo mara zote, jamii ya kimataifa imekaa kimya kuhusiana na jinai hizo kwani jamii hiyo imedhibitiwa na Marekani. Mbunge huyo Msuni katika Bunge la Iran ameongeza kwamba: Kundi la Daesh ambalo limeundwa na Marekani, limefanya mauaji na jinai kubwa dhidi ya wananchi wa Syria lakini Marekani hiyo hiyo inajitokeza hadharani na kuthubutu kusema kuwa inaunga mkono haki za binadamu. Mbunge huo ameashiria uungaji mkono wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa wananchi Wakurdi wa Iraq na kuongeza kwamba serikali ya Uturuki si tu kwamba haiwasaidii wananchi Wakurdi wa Kobani huko Syria, bali hata inazuia kuwafikia misaada ya kibinadamu wananchi hao.

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com