Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Wednesday, October 8

Mjumbe UN asisitiza suala la kulindwa raia S/Kusini

Posted by mkachu  |  Tagged as:

Mjumbe UN asisitiza suala la kulindwa raia S/KusiniMwakilishi mpya wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini ametaka zifanyike juhudi kubwa za kulindwa usalama wa raia wa nchi hiyo. Ellen Margrethe Loej ambaye ameteuliwa hivi karibuni kuwa mjumbe mpya wa Ban Ki moon Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini amesema kwamba, atalipa kipaumbele suala la kulindwa usalama wa raia, na kusisitiza kwamba Sudan Kusini linakabiliwa na changamoto nyingi likiwemo suala la wimbi la wakimbizi. Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini ameongeza kuwa, kuna ulazima wa kutumiwa suhula zaidi kwa lengo la kudhaminiwa mahitajio ya watu wanaohitajia misaada ya kibinadamu. Ellen Loej amesisitiza kwamba watu waliotenda jinai za kivita au zilizo dhidi ya binadamu wanapaswa kuchukuliwa hatua za kisheria. Inafaa kuashiria hapa kuwa, machafuko nchini Sudan Kusini yalianza mwezi Disemba mwaka jana, na hadi sasa viongozi wa serikali ya Juba na waasi wanaoongozwa na Riek Machar makamu wa zamani wa rais wameshatiliana saini makubaliano ya amani mara nne, lakini makubaliano hayo yamekuwa yakikiukwa na pande hizo mbili. Shirika la Mpango wa Chakula Duniani WFP limetangaza kuwa, watu zaidi ya milioni moja na nusu wa nchi hiyo wamelazimika kuwa wakimbizi ndani na nje ya nchi hiyo.
 

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com