Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Wednesday, October 8

Kenyatta ahudhuria vikao vya Mahakama ya ICC

Posted by mkachu  |  Tagged as:

Kenyatta ahudhuria vikao vya Mahakama ya ICCUhuru Kenyatta leo amehudhuria kikao maalumu cha Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC iliyoko nchini Uholanzi, kwa lengo kujibu tuhuma zinazomkabili za kuhusika kwenye machafuko yaliyotokea baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2007 nchini Kenya. Kwenye vikao vilivyofanyika mahakamani, Kenyatta ameonekana akiwa makini kumsikiliza mwendesha mashtaka wa ICC na wakati mwingine alionekana kuwa ni mwenye mfadhaiko. Mwendesha Mashtaka wa ICC amesema kuwa, Kenyatta hakutoa ushirikiano wa kutosha kwa mahakama hiyo wakati wa kufuatilia rekodi zake za ulipaji kodi,rekodi za simu na taarifa za kibenki. Kenyatta amesema kuwa, mashtaka yaliyofunguliwa dhidi yake ni ya kisiasa na kusisi tiza kwamba kesi hiyo inapaswa kufutwa. Uhuru Kenyatta ambaye aliamua kutangaza kujiengua kwenye wadhifa wake wa urais kwa shabaha ya kushiriki kwenye vikao vya mahakama ya ICC, anakabiliwa na mashtaka matano yaliyosababisha kuibuka machafuko na ghasia zilizotokea baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2007, na kusababisha watu 1,200 kuuawa na wengine 600,000 kuyahama makazi yao.

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com