Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Wednesday, October 8

Wahubiri wenye misimamo mikali kutoingia Australia

Posted by mkachu  |  Tagged as:

Wahubiri wenye misimamo mikali kutoingia AustraliaSerikali ya Australia imepiga marufuku kuingia nchini humo wahubiri wa dini ya Kiislamu wenye misimamo ya kufurutu mipaka. Tony Abbott Waziri Mkuu wa Australia amesema kuwa, ofisi za ubalozi za nchi hiyo zimepewa jukumu la kuhakikisha wanadhibiti utoaji viza kwa wahubiri wenye misimamo mikali kuingia nchini humo. Abbott amesisitiza kwamba, hakuna haja kwa sheria hiyo kupitishwa bungeni. Msimamo wa serikali ya Australia umechukuliwa baada ya mhubiri mmoja kutoka kundi la Hizbul Tahrir kutoa matamshi makali wiki iliyopita mjini Sydney kwamba, wanataka kuweka dola la Kiislamu nchini humo. Waziri Mkuu wa Australia ameongeza kuwa, hatua ya kupiga marufuku kuingia nchini humo wahubiri wenye m isimamo mikali ina lengo la kuzuia kujitokeza uadui, chuki na mifarakano kati ya wananchi wa nchi hiyo.

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com