Leo ni Jumatano tarehe 13 Dhilhaji 1435 Hijria sawa na tarehe 8 Oktoba 2014.
Siku kama ya leo miaka 1436
iliyopita, sawa na tarehe 13 Dhilhaji mwaka mmoja kabla ya Mtume Mtukufu
(S.A.W) kuhamia Madina, yalifanyika makubaliano muhimu ya pili ya
Aqabah, kati ya Mtume Mtukufu (saw) na kundi la watu wa mji wa Yathrib
ambao baadaye ulijulikana kwa jina la sasa la Madina. Makubaliano hayo
yalifuatia makubaliano ya awali yaliyofanyika siku chache kabla. Vita
vya muda mrefu kati ya makabila mawili ya Aus na Khazraj katika mji wa
Yathrib, vilikuwa sababu ya kutafutwa mtu mwaminifu atakayeweza
kurejesha amani na utulivu kati ya pande hizo mbili. Kwa utaratibu huo
watu wa Yathrib yaani Madina ya sasa, walimtaka Mtume Muhammad (saw)
aende kwenye mji wao ili kuwasuluhisha na kuunga tena udugu baina yao.
Watu wa Yathrib pia walifunga mkataba wa
kumhami Mtume hadi tone la
mwisho la damu yao. Mkataba wa Aqabah ulikuwa na umuhimu mkubwa katika
historia ya Uislamu na ulitayarisha uwanja wa Mtume (saw) na Waislamu
kuhamia Madina wakitokea Makka na kufungua ukurasa mpya wa kueneza dini
ya Uislamu.
Siku kama ya leo miaka 24
iliyopita, kwa mara nyingine tena utawala haramu wa Israel ulifanya
jinai nyingine ya kinyama kwa kuwashambulia waumini wa Kipalestina
waliokuwa wakisali ndani ya Msikiti mtukufu wa al-Aqsa huko Palestina
inayokaliwa kwa mabavu. Wapalestina 20 waliuawa shahidi na makumi ya
wengine kujeruhiwa. Mauaji ya Wapalestina yaliyofanywa na utawala
ghasibu wa Israel tena ndani ya Msikiti wa al-Aqsa, kwa mara nyingine
tena yalilipua ghadhabu za walimwengu dhidi ya utawala huo katili. Hata
hivyo kama kawaida, uungaji mkono wa Marekani kwa Israel ulizuia
kuchukuliwa hatua yoyote ya kivitendo dhidi ya utawala huo.
Na miaka 9 iliyopita katika
siku kama ya leo, mtetemeko mkubwa wa ardhi uliokuwa na ukubwa wa 7.8
kwa kipimo cha Rishta uliyakumba maeneo ya kaskazini mashariki mwa
Pakistan. Kitovu cha mtetemeko huo kilikuwa katika mji wa Muzaffarabad.
Watu karibu 90,000 walipoteza maisha yao na wengine 3,300,000 kubaki
bila makazi.

Facebook
Twitter
RSS
0 toamaon yako: