Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Wednesday, October 8

Jumatano, Oktoba 8, 2014

Posted by mkachu  |  Tagged as:

Leo ni Jumatano tarehe 13 Dhilhaji 1435 Hijria sawa na tarehe 8 Oktoba 2014.
Jumatano, Oktoba 8, 2014Siku kama ya leo miaka 1436 iliyopita, sawa na tarehe 13 Dhilhaji mwaka mmoja kabla ya Mtume Mtukufu (S.A.W) kuhamia Madina, yalifanyika makubaliano muhimu ya pili ya Aqabah, kati ya Mtume Mtukufu (saw) na kundi la watu wa mji wa Yathrib ambao baadaye ulijulikana kwa jina la sasa la Madina. Makubaliano hayo yalifuatia makubaliano ya awali yaliyofanyika siku chache kabla. Vita vya muda mrefu kati ya makabila mawili ya Aus na Khazraj katika mji wa Yathrib, vilikuwa sababu ya kutafutwa mtu mwaminifu atakayeweza kurejesha amani na utulivu kati ya pande hizo mbili. Kwa utaratibu huo watu wa Yathrib yaani Madina ya sasa, walimtaka Mtume Muhammad (saw) aende kwenye mji wao ili kuwasuluhisha na kuunga tena udugu baina yao. Watu wa Yathrib pia walifunga mkataba wa kumhami Mtume hadi tone la mwisho la damu yao. Mkataba wa Aqabah ulikuwa na umuhimu mkubwa katika historia ya Uislamu na ulitayarisha uwanja wa Mtume (saw) na Waislamu kuhamia Madina wakitokea Makka na kufungua ukurasa mpya wa kueneza dini ya Uislamu.
Siku kama ya leo miaka 24 iliyopita, kwa mara nyingine tena utawala haramu wa Israel ulifanya jinai nyingine ya kinyama kwa kuwashambulia waumini wa Kipalestina waliokuwa wakisali ndani ya Msikiti mtukufu wa al-Aqsa huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu. Wapalestina 20 waliuawa shahidi na makumi ya wengine kujeruhiwa. Mauaji ya Wapalestina yaliyofanywa na utawala ghasibu wa Israel tena ndani ya Msikiti wa al-Aqsa, kwa mara nyingine tena yalilipua ghadhabu za walimwengu dhidi ya utawala huo katili. Hata hivyo kama kawaida, uungaji mkono wa Marekani kwa Israel ulizuia kuchukuliwa hatua yoyote ya kivitendo dhidi ya utawala huo.
Na miaka 9 iliyopita katika siku kama ya leo, mtetemeko mkubwa wa ardhi uliokuwa na ukubwa wa 7.8 kwa kipimo cha Rishta uliyakumba maeneo ya kaskazini mashariki mwa Pakistan. Kitovu cha mtetemeko huo kilikuwa katika mji wa Muzaffarabad. Watu karibu 90,000 walipoteza maisha yao na wengine 3,300,000 kubaki bila makazi.

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com