Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Wednesday, October 8

'Umoja ndio utakaokomesha misimamo mikali Iraq'

Posted by mkachu  |  Tagged as:

'Umoja ndio utakaokomesha misimamo mikali Iraq'Spika wa Majilisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema kuwa umoja na mshikamano kati ya makundi ya kisiasa nchini Iraq ndio unaoweza kukomesha misimamo mikali na machafuko katika nchi hiyo ya Kiarabu. Ali Larijani amesema hayo leo wakati alipoonana na Waziri wa Vijana na Michezo wa Iraq Abdul Huddein Abrani hapa mjini Tehran na kuongeza kuwa, umoja wa kitaifa na mshikamano kati ya makundi ya kisiasa ya Iraq unao uwezo wa kuzuia kuenea machafuko na makundi yenye misimamo mikali nchini Iraq. Kiongozi huyo wa juu kabisa katika Bunge la Iran ameongeza kuwa, ana matumaini kuundwa serikali mpya Iraq kutafungua njia ya kudumishwa amani na kupambana vilivyo na makundi ya kigaidi nchini humo. Amesema, uongozi mzuri wa wanasiasa nchini Iraq na kuundwa serikali mpya nchini humo kunaweza kupunguza matatizo waliyo nayo wananchi wa Iraq hivi sasa. Kwa upande w ake Bw. Abdul Hussein Abtan, Waziri wa Vijana na Michezo wa Iraq ameishukuru serikali na wananchi wa Iran kwa uungaji mkono wao kwa taifa la Iraq na kuongeza kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran daima imekuwa muungaji mkono wa mapambano dhidi ya ugaidi na kudumishwa amani na utulivu nchini Iraq na kwamba wananchi wa Iraq kamwe hawawezi kusahau msaada huo wa wananchi na serikali ya Iran kwao.

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com