Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Wednesday, October 8

'Ripoti haki za binadamu kuhusu Iran haina mashiko'

Posted by mkachu  |  Tagged as:

'Ripoti haki za binadamu kuhusu Iran haina mashiko'Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa, ripoti ya hivi karibuni ya mjumbe maalumu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa kuhusiana na Iran umetolewa bila ya kuzingatia sheria na majukumu ya wafanyakazi wa baraza la haki za binadamu na haina uzito wowote wa kisheria.
Bi Marzie Afkham amesema hayo leo Jumatano mbele ya waandishi wa habari na kuongeza kuwa, ripoti ya Ahmed Shaheed, mjumbe maalumu wa baraza la haki za binadamu la Umoja wa Mataifa kuhusiana na Iran imeangalia mambo kwa upande mmoja na hayana ukweli wowote. Ameongeza kuwa, Ahmed Shaheed kimsingi amekuwa mwendesha siasa zilizo dhidi ya Iran.
Amma kuhusiana na duru ijayo ya mazungumzo ya nyuklia na kundi la 5+1 Bi. Afkham amesema, mazungunzo ya pande mbili na pande kadhaa baina ya Iran na kundi hilo yataendelea wiki ijayo huko Vienna, Uswisi.
 

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com