Baada ya kufikiwa makubaliano kati ya serikali na vyama vya kisiasa vya
Yemen kuhusu kuundwa serikali mpya, Rais Abd Rabbuh Mansur Hadi wa nchi
hiyo amempa jukumu la kuunda serikali Ahmed Awadh bin Mubarak aliyekuwa
mkuu wa ofisi ya rais. Lakini hivi sasa uteuzi huo umekumbwa na utata.
Hii ni kwa sababu harakati ya Ansarullah na chama cha Kongresi ya Taifa
ya Ukombozi wa Yemen vimepinga kuchaguliwa uteuzi huo. Kabla ya
makubaliano hayo ilikubaliwa kuwa, uteuzi wa waziri mkuu mpya ufanyike
kwa maafikiano ya vyama vyote na makundi ya kisiasa ya Yemen. Ingawa
makamu wa rais wa Yemen ametangaza kuwa uteuzi wa Mubarak kama waziri
mkuu mpya umefanyika baada ya maafikiano ya vyama vyote, lakini ushahidi
uliopo ni kinyume na madai hayo. Wachambuzi wengi wa masuala ya kisiasa
wanaamini kuwa, iwapo harakati ya Ansarullah itaendelea kupinga
kuteuliwa bin Mubarak kuwa waziri mkuu, suala hilo linaweza kuandaa
mazingira ya kuibuka mgogoro mpya nchini Yemen. Hasa kwa kuzingatia
kuwa, pande mbili za mgogoro wa Yemen ambazo ni serikali na harakati ya
Ansarullah bado haziaminiani. Suala hilo linadhihirishwa wazi na msimamo
uliochukuliwa hivi karibuni wa harakati ya Answarullah. Harakati hiyo
inasema kuwa, uteuzi wa Bw. Ahmad Awadh bin Mubarak aliyepewa jukumu la
kuunda serikali mpya ya Yemen umefanyika baada ya kufanyika mazungumzo
baina ya balozi wa Marekani
na Rais Abdu Rabuh Mansur Hadi. Hii
inaamanisha kuwa, viongozi wa Washington wana nafasi katika kuainisha
waziri mkuu mpya wa Yemen. Harakati ya Ansarullah imetangaza rasmi kuwa,
uteuzi wa bin Mubarak haukufanywa ndani ya nchi. Kwa ajili hiyo kundi
hilo halitaki kwa mara nyingine Abdu Rabah Mansur Hadi ampe jukumu la
kuunda Baraza la Mawaziri mtu ambaye amechaguliwa na Wamagharibi. Hivi
karibuni hali ya Yemen ilikuwa ni ya kimapinduzi. Wananchi wa nchi hiyo
walijitokeza mabarabarani na kupiga nara za kutaka Rais Abd Rabbuh
Mansur Hadi aondoke madarakani na serikali yake ibadilishwe. Mwishowe
kutokana na mashinizo ya walio wengi na kwa mujibu wa makubaliano
yaliyofikiwa chini ya upatanishi Umoja wa Mataifa kati ya Ansaruddin na
serikali ya Sana'a, Abdu Rabbuh alikubali kubadilisha serikali.
Walikubaliana kuwa serikali mpya iundwe na waziri mkuu atakayeafikiwa na
vyama vyote vya kisiasa. Lakini kwa kuwa hakuna kuaminiana kati ya
pande hizo mbili, kuna swali linalojitokeza hapa kwamba, je, makundi ya
Yemen yanaweza kumuarifisha waziri mkuu atayakayekubaliwa na pande zote?
Hapana shaka kuwa suala hilo linaweza kufanikiwa iwapo mitazamo ya
vyama vyenye taathira na viongozi wanaotawala Yemen kuhusu kuundwa
serikali itakakaribiana. Kwa kuzingatia kuwa Marekani inataka kuwa na
nafasi kubwa zaidi katika maamuzi ya Yemen, je, kuna matumaini ya
kuundwa serikali ya kitaifa itakayoafikiwa na makundi yote nchini humo?
Kwa kuzingatia kuwa mtazamo wa serikali ya Sana'a na harakati ya
Answarullah kuhusiana na Wamagharibi unatofautiana, ni wazi kuwa, suala
hilo ni jambo gumu kwa Yemen. Iwapo pande za nchi hiyo hazitoafikiana
haraka kuhusu nafasi ya waziri mkuu, kuna uwezekano matukio mapya
yakashuhudiwa nchini Yemen, ambapo kuvunjwa makubaliano ya usitishaji
vita ni matokeo mabaya zaidi ya suala hilo.
IQRA FM RADIO
Wednesday, October 8
Browse: Home
» Habari za kitaifa na kimataifa
» Kundi la Ansarullah lapinga uteuzi wa waziri mkuu mpya wa Yemen
Kundi la Ansarullah lapinga uteuzi wa waziri mkuu mpya wa Yemen
Posted by mkachu |  Tagged as: Habari za kitaifa na kimataifa
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Andika Maoni
add
LEO KATIKA HISTORIA
TANGAZANASI
kwama Matangazo wasiliana nasi kupitia anuani zifuataz
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
ZILIZO SOMWA ZAIDI
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa ni dua za baada ya nyakati mbalimbali za sala. Tunamuomba Mwenyezi Mung...
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa chini ni dua 25 za Qur'ani Tukufu tulizozinukuu kutoka katika...
-
RATIBA YA VIPINDI KWA JUMA ZIMA RATIBA - JUMATATU MUDA KIPINDI MUHUSIKA 06:30-07:00 M...
-
Rais Bashar al-Assad wa Syria amesema kuwa, kuna udharura wa kuweko vita vya kimataifa dhidi ya magaidi. Rais Assad amesisitiza kwamba, kwa...
MITANDAO YA KIJAMII
TAFUTA HABARI ZILIZO SOMWA NYUMA
Powered by Blogger.
Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...
0 toamaon yako: