Mshauri wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu katika masuala
ya kimataifa amezikosoa vikali siasa za kindumakuwili za Marekani na
kubainisha kwamba, Washington haitasimama na kupambana na ugaidi. Dakta
Ali Akbar Velayati amesema bayana kwamba, nchi kama Marekani ambazo
zimetanguliza mbele siasa za kindumakuwili katika Mashariki ya Kati,
bila shaka haziwezi kuja na kuanza kupambana na ugaidi.
Dakta Velayati ambaye pia ni Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa
Kiisratijia ya Halmashauri ya Kuainisha Maslahi ya Mfumo wa Jamhuri ya
Kiislamu ya Iran amesema hayo alipokutana hapa mjini Tehran na Ujumbe wa
Taasisi ya Utafiti wa Kielimu kutoka Sweden na kueleza masikitiko yake
kutokana na uingiliaji kati wa madola ya kigeni katika masuala ya eneo
hili la
Mashariki ya Kati.
Amesema, madola yanayofanya uingiliaji katika masuala ya Mashariki ya
Kati yanalipeleka eneo hili upande wa kuangamia. Mshauri wa Kiongozi
Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kwamba, madola kama Marekani
na waitifaki wake ambao wanapigia upatu suala la kupambana na ugaidi na
wakati huohuo kuendesha siasa za kindumakuwili katu hayawezi kuwa na nia
ya kweli na ya dhati katika kupambana na ugaidi.
IQRA FM RADIO
Monday, October 13
Velayati: Marekani haitasimama kupambana na ugaidi
Posted by mkachu |  Tagged as: Habari za kitaifa na kimataifa
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Andika Maoni
add
LEO KATIKA HISTORIA
TANGAZANASI
kwama Matangazo wasiliana nasi kupitia anuani zifuataz
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
ZILIZO SOMWA ZAIDI
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa ni dua za baada ya nyakati mbalimbali za sala. Tunamuomba Mwenyezi Mung...
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa chini ni dua 25 za Qur'ani Tukufu tulizozinukuu kutoka katika...
-
RATIBA YA VIPINDI KWA JUMA ZIMA RATIBA - JUMATATU MUDA KIPINDI MUHUSIKA 06:30-07:00 M...
-
Rais Bashar al-Assad wa Syria amesema kuwa, kuna udharura wa kuweko vita vya kimataifa dhidi ya magaidi. Rais Assad amesisitiza kwamba, kwa...
MITANDAO YA KIJAMII
TAFUTA HABARI ZILIZO SOMWA NYUMA
Powered by Blogger.
Author
CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

Facebook
Twitter
RSS
0 toamaon yako: