Dakta Ali Larijani Spika wa Majlis ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la
Iran) jana aliongoza ujumbe wa ngazi za juu wa bunge kwa shabaha ya
kushiriki kikao cha 131 cha Muungano wa Mabunge Duniani kinachoanza leo
mjini Geneva, Uswisi. Hapo jana, Dakta Larijani alishiriki kikao cha
Jumuiya ya Mabunge ya Asia na Pasifiki mjini Geneva.
Kikao cha mwaka huu cha Muungano wa Mabunge Duniani kinafanyika huku
ulimwengu ukishuhudia kuongezeka vita, mapigano na harakati za makundi
ya kigaidi ambazo zinatishia amani na utulivu duniani. Mabunge yakiwa ni
mhimili uliochaguliwa na wananchi, yanaweza kuwa na nafasi kubwa ya
kuimarisha mashirikiano kati ya mataifa, utamaduni na dini mbalimbali
kwa lengo la kutatua matatizo na kukabiliana na vitisho vilivyopo. Kwa
minajili hiyo, masuala kama vile haki za binadamu, ugaidi, ukandamizaji,
uchupaji mipaka, amani na usalama duniani ni miongoni mwa ajenda kuu
zinazotarajiwa kujadiliwa kwa kina kwenye kikao hicho. Amma swali
linalojitokeza hapa ni hili kwamba, je mabunge yanaweza kuwa na uwezo wa
kuchukua hatua mwafaka katika kutatua matatizo na kero zilizopo? Au
kikao hicho cha Geneva kitaweza kuwa na fikra za pamoja na kuchukua
maamuzi yasiyokuwa ya kimaonyesho kwa lengo la kukabiliana na ugaidi na
matatizo yanayoukumba ulimwengu kwa hivi sasa?
Hakuna shaka kwamba, sharti la kwanza katika kufanikiwa jambo hilo,
ni kwa nchi zote kukiri kwamba zinakabiliwa na tishio la makundi ya
kigaidi. Hata hivyo jukumu la mabunge hayo la kukabiliana na ugaidi
linakuwa hata gumu zaidi pale tunapotambua kuwa, baadhi ya nchi licha ya
kukabiliwa na upinzani wa wananchi wao, zimekuwa zikiyaunga mkono moja
kwa moja makundi hayo kwa kisingizio cha eti kupambana na ugaidi. Ukweli
huo mchungu unashuhudiwa kwa Marekani na baadhi ya washirika wake
kutoka Ulaya pamoja na nchi za Kiarabu ambazo zinatoa bila kusita
misaada ya fedha, silaha na uungaji mkono wao kwa makundi ya kigaidi. Na
ndiyo maana leo hii tunashuhudia vitisho na harakati za ugaidi
zikipamba moto ulimwenguni kote.
Leo hii magaidi wanapanda mbegu za ghasia na machafuko sanjari na
kufuta utamaduni na thamani za kidini na kibinadamu duniani. Katika hali
kama hii tata na nyeti inatazamiwa kuwa, mabunge yakiwa ni asasi ya
wananchi yataweza kulichukulia suala hili kwa uzito mkubwa bila ya
kuathiriwa na mirengo ya kisiasa. Hivi sasa ulimwengu unashuhudia raia
wa Ulaya wakiwa wamejiunga na makundi ya kigaidi, na kufanya mauaji ya
kutisha katika nchi za eneo la Mashariki ya Kati zikiwemo Syria na Iraq.
Kuendelea kwa harakati za kigaidi, kunaweza kusababisha majanga na
maafa makubwa duniani. Hivi sasa jamii ya kimataifa bado haijaweza kuwa
na mtazamo wa pamoja na unaokubalika kuhusiana na maan
a halisi ya neno
ugaidi, hivyo mabunge yanapaswa kutoa mchango wao mkubwa ili nchi zote
zishirikiane katika kutokomeza ugaidi duniani. Muungano wa Mabunge
Duniani ikiwa ni asasi huru, unapaswa kuhifadhi uhuru wake na kutekeleza
majukumu yake kwa ufanisi mkubwa bila ya woga.
Mojawapo ya changamoto kubwa zinazozikabili taasisi za kimataifa ni
kuwa tegemezi na kukubali kuathiriwa na madola makubwa duniani. Kwa
mfano taasisi kama vile Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa
na Benki ya Dunia zimekuwa zikiathiriwa na mirengo ya kisiasa na
kusababisha nguvu na ushawishi wa taasisi hizo kudhoofika. Kwa minajili
hiyo tunataraji kuona Muungano wa Mabunge Duniani ukifuata nyayo za hati
ya Umoja wa Mataifa katika kusaidia kutatua migogoro kiadilifu na
kuchukua hatua madhubuti za kuzuia kuongezeka vitisho; suala ambalo
Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imelipendekeza kwenye kikao cha mwaka huu
mjini Geneva. Ujumbe wa Bunge la Iran umetoa pendekezo lijulikanalo;
'Jukumu la Muungano wa Mabunge Duniani ni kufungamana na hati ya Umoja
wa mataifa katika kutatua migogoro kwa uadilifu na usawa na kuchukua
hatua madhubuti za kukabiliana na ongezeko la tishio la ugaidi duniani'.
IQRA FM RADIO
Monday, October 13
Browse: Home
» Habari za kitaifa na kimataifa
» Bunge la Kimataifa; ni fursa nzuri ya kuwepo fikra za pamoja duniani
Bunge la Kimataifa; ni fursa nzuri ya kuwepo fikra za pamoja duniani
Posted by mkachu |  Tagged as: Habari za kitaifa na kimataifa
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Andika Maoni
add
LEO KATIKA HISTORIA
TANGAZANASI
kwama Matangazo wasiliana nasi kupitia anuani zifuataz
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
ZILIZO SOMWA ZAIDI
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa ni dua za baada ya nyakati mbalimbali za sala. Tunamuomba Mwenyezi Mung...
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa chini ni dua 25 za Qur'ani Tukufu tulizozinukuu kutoka katika...
-
RATIBA YA VIPINDI KWA JUMA ZIMA RATIBA - JUMATATU MUDA KIPINDI MUHUSIKA 06:30-07:00 M...
-
Rais Bashar al-Assad wa Syria amesema kuwa, kuna udharura wa kuweko vita vya kimataifa dhidi ya magaidi. Rais Assad amesisitiza kwamba, kwa...
MITANDAO YA KIJAMII
TAFUTA HABARI ZILIZO SOMWA NYUMA
Powered by Blogger.
Author
CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

Facebook
Twitter
RSS
0 toamaon yako: