Profesa Ali Mazrui, msomi mashuhuri wa Afrika na duniani kwa ujumla wa
nchini Kenya amefariki dunia leo. Profesa Mazrui msomi mtajika,
aliyekuwa na umri wa miaka 81, amefariki dunia leo Jumatatu nchini
Marekani alikokuwa akiishi baada ya kuugua kwa muda wa miezi kadhaa.
Khelef Khalifa Mwenyekiti wa Shirika la Kiislamu la Kutetea Haki za
Binadamu nchini Kenya (MUHURI) amesema kuwa, mwili wa marehemu Profesa
Ali Alamin Mazrui utasafirishwa na kupelekwa Kenya kwa ajili ya mazishi.
Alamin Mazr
ui ambaye ni mpwa wa mwendazake Profesa Ali Mazrui
amethibitisha kwamba, marehemu alipenda azikwe nchini Kenya. Profesa
Mazrui alikuwa msomi wa masuala ya kisiasa, utamaduni wa Kiafrika na
masuala ya dini ya Kiislamu na alisifika sana kwa kuangazia utamaduni wa
Kiafrika kwa walimwengu. Alizaliwa Februari 24 mwaka 1933 huko Mombasa,
Kenya na hadi anaaga dunia alikuwa mhadhiri katika Chuo Kikuu cha
Binghamton huko New York Marekani. Msomi huyo alikuwa pia mwandishi na
ameandika vitabu visivyopungua 30. Marehemu amaecha mke na watoto sita
IQRA FM RADIO
Monday, October 13
Prof. Mazrui, msomi mashuhuri Afrika afariki dunia
Posted by mkachu |  Tagged as: Habari za kitaifa na kimataifa
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Andika Maoni
add
LEO KATIKA HISTORIA
TANGAZANASI
kwama Matangazo wasiliana nasi kupitia anuani zifuataz
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
ZILIZO SOMWA ZAIDI
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa ni dua za baada ya nyakati mbalimbali za sala. Tunamuomba Mwenyezi Mung...
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa chini ni dua 25 za Qur'ani Tukufu tulizozinukuu kutoka katika...
-
RATIBA YA VIPINDI KWA JUMA ZIMA RATIBA - JUMATATU MUDA KIPINDI MUHUSIKA 06:30-07:00 M...
-
Rais Bashar al-Assad wa Syria amesema kuwa, kuna udharura wa kuweko vita vya kimataifa dhidi ya magaidi. Rais Assad amesisitiza kwamba, kwa...
MITANDAO YA KIJAMII
TAFUTA HABARI ZILIZO SOMWA NYUMA
Powered by Blogger.
Author
CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

Facebook
Twitter
RSS
0 toamaon yako: