Rais Evo Morales wa Bolivia amechaguliwa tena kwa mara ya tatu
kuiongoza nchi hiyo ya Amerika ya Kusini baada ya kuibuka mshindi katika
uchaguzi wa Rais uliofanyika jana nchini humo. Morales ambaye ni mfuasi
wa siasa za mrengo wa kushoto na anayehesabiwa kuwa mpinzani mkuu wa
ubeberu amejipatia ushindi wa asilimia 61 ya kura na hivyo kuibuka
mshindi wa kiti cha Urais katika duru ya kwanza tu ya uchaguzi huo.
Mfanyabiashara mashuhuri nchini humo Samuel Doria Medina
aliyekuwa akichuana na Evo Morales ameambulia asilimia
24 ya kura. Mbali
na uchaguzi wa Rais, jana wananchi wa Bolivia waliwachagua pia
wawakilishi wa Bunge na wale wa Baraza la Seneti. Matokeo ya awali
yanaonesha kuwa, chama cha Morales kimefanikiwa pia kupata wingi wa viti
vya Bunge na Baraza la Seneti. Akizungumza kwenye hotuba ya kuwashukuru
wapiga kura, Morales alisema ushindi huo mkubwa unamaanisha imani kubwa
waliyonayo Wabolivia kwa sera zake dhidi ya ubepari, ubeberu na
ukoloni.
IQRA FM RADIO
Monday, October 13
Rais Evo Morales achaguliwa tena kuiongoza Bolivia
Posted by mkachu |  Tagged as: Habari za kitaifa na kimataifa
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Andika Maoni
add
LEO KATIKA HISTORIA
TANGAZANASI
kwama Matangazo wasiliana nasi kupitia anuani zifuataz
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
ZILIZO SOMWA ZAIDI
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa ni dua za baada ya nyakati mbalimbali za sala. Tunamuomba Mwenyezi Mung...
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa chini ni dua 25 za Qur'ani Tukufu tulizozinukuu kutoka katika...
-
RATIBA YA VIPINDI KWA JUMA ZIMA RATIBA - JUMATATU MUDA KIPINDI MUHUSIKA 06:30-07:00 M...
-
Rais Bashar al-Assad wa Syria amesema kuwa, kuna udharura wa kuweko vita vya kimataifa dhidi ya magaidi. Rais Assad amesisitiza kwamba, kwa...
MITANDAO YA KIJAMII
TAFUTA HABARI ZILIZO SOMWA NYUMA
Powered by Blogger.
Author
CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

Facebook
Twitter
RSS
0 toamaon yako: