Leo ni Jumapili tarehe 10 Dhul-Hijja mwaka 1435 Hijria, sawa na tarehe 5 Oktoba mwaka 2014 Miladia.
Leo
tarehe 10 Dhilhaj ni sikukuu ya Idul Adh'ha, moja ya sikukuu kubwa za
Kiislamu. Katika siku hii mahujaji wa Nyumba Tukufu ya Mwenyezi Mungu
waliokwenda Makka, huchinja mnyama kwa ajili ya kutekeleza amri ya Mola
wao na kuhuisha kumbukumbu ya Nabii Mtukufu Ibrahim (as). Mwenyezi Mungu
aliijaribu imani na ikhlasi ya Nabii huyo kwa kumuamuru amchinje
mwanawe kipenzi Ismail (as). Licha ya mashaka ya utekelezwaji wa amri
hiyo, Nabii Ibrahimu (as) aliandaa mazingira ya utekelezwaji wake na
kumlaza chini mwanaye huyo na kuanza kuikata shingo yake lakini kisu
kilikataa kuchinja. Hapo
ndipo akaambiwa na Mwenyezi Mungu kuwa amefaulu
mtihani huo na akamtumia mnyama wa kuchinja badala ya mwanaye Ismail.
Tukio hili lenye ibra na mafunzo tele linawapa wanadamu somo la kujitoa
mhanga, kujisabilia kwa ajili ya Allah, kushinda matamanio na matakwa ya
nafsi na kusalimu amri mbele ya amri za Mwenyezi Mungu Mtukufu. Redio
Tehran inatoa mkono wa baraka na fanaka kwa Waislamu kote duniani kwa
mnasaba wa sikukuu hii kubwa.
Siku kama ya leo miaka 36 iliyopita,
Imam Khomeini (MA) Mwasisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran alihama Iraq
na kuelekea Paris Ufaransa. Imam Khomeini aliamua kufanya hijra hiyo ya
kihistoria wakati utawala wa zamani wa Iraq ulipoanza kumzuia ache
harakati zake za mapambano dhidi ya utawala wa Shah. Serikali ya wakati
huo ya Iraq ambayo ilikuwa ikilinda mahusiano na utawala wa Shah nchini
Iran, ilimtaka Imam Khomeini ajiepushe na harakati zozote za kisiasa na
za kimapinduzi dhidi ya utawala huo wa Shah. Hata hivyo Imam aliimbia
serikali hiyo kuwa hilo lilikuwa ni jukumu lake la kisheria ambalo
aliwajibika kulitekeleza na kusisitiza juu ya kuendeleza mapambano yake
kwa kutoa hotuba na kutuma kanda za kimapinduzi nchini Iran.
Siku
kama ya leo miaka 14 iliyopita, Slobodan Milosevic dikteta wa Yugoslavia
na muhusika mkuu wa vita vya umwagaji damu huko Balkan, alijiuzulu
baada ya miezi kadhaa ya malalamiko ya ndani na vikwazo vya kimataifa.
Milosevic alikuwa rais wa Serbia tangu mwaka 1990 hadi 1997 na baadaye
akawa rais wa Jamhuri ya Yugoslavia. Katika vita vya Bosnia, na kwa
uungaji mkono wa kila upande wa Waserbia, Slobodan Milosevic alishiriki
pakubwa katika kutekeleza mauaji ya kizazi dhidi ya Waislamu wa Bosnia.
Slobodan Milosevic alikuwa kiongozi wa kwanza mtenda jinai za kivita
kuwahi kufikishwa katika mahakama ya kimataifa kwa ajili ya kuhukumiwa.
Na
siku kama ya leo miaka 150 iliyopita, alizaliwa Louis Jean Lumiere,
mwanakemia mwanaviwanda mashuhuri wa Kifaransa. Mwaka 1895 akiwa pamoja
na ndugu yake, aliyejulikana kwa jina la Auguste Lumiere, walifanikiwa
kutengeneza kifaa ambacho kiliwasaidia kuchukua picha mbalimbali na
kusajili harakati. Mwaka huo huo Lumiere alifanikiwa kuonyesha filamu
yake ya kwanza au Motion Picture katika majumba ya sinema.
IQRA FM RADIO
Wednesday, October 8
Jumapili, 05 Oktoba, 2014
Posted by mkachu |  Tagged as: leo katka hisory
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Andika Maoni
add
LEO KATIKA HISTORIA
TANGAZANASI
kwama Matangazo wasiliana nasi kupitia anuani zifuataz
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
ZILIZO SOMWA ZAIDI
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa ni dua za baada ya nyakati mbalimbali za sala. Tunamuomba Mwenyezi Mung...
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa chini ni dua 25 za Qur'ani Tukufu tulizozinukuu kutoka katika...
-
RATIBA YA VIPINDI KWA JUMA ZIMA RATIBA - JUMATATU MUDA KIPINDI MUHUSIKA 06:30-07:00 M...
-
Rais Bashar al-Assad wa Syria amesema kuwa, kuna udharura wa kuweko vita vya kimataifa dhidi ya magaidi. Rais Assad amesisitiza kwamba, kwa...
MITANDAO YA KIJAMII
TAFUTA HABARI ZILIZO SOMWA NYUMA
Powered by Blogger.
Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...
0 toamaon yako: