Leo ni Jumamosi tarehe 9 Mfunguo Tatu Dhil-Hija mwaka 1435 Hijria mwafaka na tarehe 4 Oktoba mwaka 2014 Miladia.
Leo ni siku ya Arafa tarehe 9 Dhil-Hija. Arafa ni jina la jangwa
kubwa linalopakana na mlima wa Jabalur Rahma ulioko kusini mashariki mwa
Makka. Tangu adhuhuri ya siku hii mahujaji wa Nyumba ya Mwenyezi Mungu
al Kaaba husimama katika uwanja wa Arafa na hadithi nyingine za Kiislamu
zimetaja fadhila na utukufu mkubwa wa kisimamo hicho. Hadithi zinasema
kuwa Mwenyezi Mungu SW ameifa
nya ardhi ya Arafa ambayo ilikuwa medani ya
matukio mengi muhimu ya kihistoria, kuwa mahala pa kuwapokea wageni
wake wanaokwenda Hija na ameweka meza na karamu yake pembeni ya mlima wa
Jabalur Rahma. Ni vyema kukumbusha kuwa magharibi ya siku hii ya leo
mahujaji wanaondoka uwanja wa Arafa na kuelekea Mash'arul Haram na
kujitayarisha kwa ajili na amali nyingine za Hija. ***
Siku kama ya leo miaka 1375 iliyopita, Muslim bin Aqil binamu wa Imam
Hussein bin Ali bin Abi Talib AS aliuawa shahidi mjini Kufa Iraq.
Alikuwa mmoja wa shakhsia wakubwa na wacha Mungu katika zama zake.
Alielekea mjini al-Kufa, Iraq akiwa na lengo la kwenda kutathmini ni kwa
kiwango gani watu wa mji huo walikuwa wakimtii Imam Hussen, baada ya
watu wa mji huo kumwandikia maelfu ya barua Imam huyo wakimtaka aende
mjini humo na kwamba wako tayari kumuunga mkono katika harakati yake
dhidi utawala dhalimu wa Yazid bin Muawiya. Watu wa Kufa walimsaliti
Muslim bin Aqil baada ya kuhadaika kwa hila na uongo wa Ubeidullah bin
Ziyad, mtawala wa wakati huo wa Kufa na wakamuacha Muslim bin Aqiil peke
yake. ***
Siku kama ya leo miaka 48 iliyopita nchi ya Kiafrika ya Lesotho
ilipata uhuru kutoka kwa mkoloni Muingereza. Kabla ya uhuru, Lesotho
ilikuwa ikijulikana kwa jina la Basutoland na kuanzia mwaka 1884 ikawa
chini ya mkoloni Mwingereza. Uingereza iliendelea kuikalia kwa mabavu
Lesotho hadi mwaka 1966 na hatimaye nchi hiyo ikapata uhuru kamili
katika siku kama ya leo. Lesotho iko kusini mwa bara la Afrika huku
ikiwa imezingirwa na jirani yake Afrika Kusini. ***
Miaka 57 iliyopita katika siku kama ya leo satalaiti ya kwanza
ilirushwa angani na msomi wa Urusi ya zamani na kwa utaratibu huo zama
za udhibiti wa anga zikaanza. Satalaiti hiyo iliyopewa jina la Sputnik 1
ilizunguka dunia mara 1400 kwa siku 92 na kwa mara ya kwanza ikafikisha
ujumbe wa radio kutoka angani kuelekea ardhini. ***
Katika siku kama ya leo miaka 184 iliyopita nchini ya Ubelgiji
ilijitangazia uhuru wake. Kuanzia karne ya 18 Ubelgiji ilikuwa chini ya
udhibiti wa Austria na mwishoni mwa karne hiyo hiyo ikawa chini ya
udhibiti wa Ufaransa. Hata hivyo baada ya Napoleone Bonaparte kushindwa
na madola ya Ulaya, mwaka 1815 Miladia, Ubelgiji na Uholanzi zilunda
muungano. Hata hivyo muungano huo haukudumu baada ya Wakatoliki wa
Ubelgiji kuanzisha uasi dhidi ya Waprotestani wa Uholanzi na kuitanga
nchi yao kuwa huru. ***
Na tarehe 4 Oktoba mwaka 1963 yaani miaka 51 iliyopita kimbunga
cheusi cha Caribbean kilianza na kuangamiza suhula zote za bandari na
visiwa vya bahari ya Caribean. Kimbunga hicho angamizi kilikuwa na kasi
ya kilomita 150 kwa saa na kwa ujumla kiliua karibu watu elfu sita wengi
wao wakiwa raia wa Cuba na Haiti. *
IQRA FM RADIO
Wednesday, October 8
Jumamosi, Oktoba 4, 2014
Posted by mkachu |  Tagged as: leo katka hisory
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Andika Maoni
add
LEO KATIKA HISTORIA
TANGAZANASI
kwama Matangazo wasiliana nasi kupitia anuani zifuataz
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
ZILIZO SOMWA ZAIDI
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa ni dua za baada ya nyakati mbalimbali za sala. Tunamuomba Mwenyezi Mung...
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa chini ni dua 25 za Qur'ani Tukufu tulizozinukuu kutoka katika...
-
RATIBA YA VIPINDI KWA JUMA ZIMA RATIBA - JUMATATU MUDA KIPINDI MUHUSIKA 06:30-07:00 M...
-
Rais Bashar al-Assad wa Syria amesema kuwa, kuna udharura wa kuweko vita vya kimataifa dhidi ya magaidi. Rais Assad amesisitiza kwamba, kwa...
MITANDAO YA KIJAMII
TAFUTA HABARI ZILIZO SOMWA NYUMA
Powered by Blogger.
Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...
0 toamaon yako: