Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Thursday, October 2

China yamuunga mkono Leung

Posted by mkachu  |  Tagged as:

Wengi wa waandamanaji ni wanafunzi wanamomtaka kiongozi wa Hong Kong kujiuzulu
China imetangaza kuunga mkono Kiongozi Mkuu wa Hong Kong, C Y Leung, anapokabiliwa na maandamano makubwa ambayo yamedumaza shughuli katika eneo kubwa la mji huo.
Wanafunzi wametisha kuanza kupiga kambi baadhi ya majengo ya Serikali iwapo kiongozi huyo hatajiuzulu ifikapo leo jioni.
Katika tahariri ya ukurasa wa mbele katika gazeti la kila siku la Kikomunisti Serikali inamuunga mkono kikamilifu na inamwamini na kuridhika na kazi yake.
Wamnempa hadi mwioshoni wa Alhamisi kufanya hivyo la sivyo wavamie majengo ya serikali
Serikali ya China pia ilionya kuwa lazima sheria na utangamano vidumishwe nchini humo au ghasia zitasambaa kila mahali.
Wandamanaji wanaendelea kushinda na kukesha katika maeneo muhimu hapo jijini kama vile pande mbili za bandari ya Hong Kong, kama hatua ya kuitisha Demokrasia zaidi.
Wanasema China inawakandamiza kwa kutaka kuwakagua wanasiasa wa Hong Kong kabla ya uchaguzi wa 2017
Idadi ya waandamanaji ni ndogo kuliko ilivyokuwa siku zilizopita lakini idadi hiyo huongezeka na kupunguka kulingana na muda.
Serikali ya China imemuunga mkono bwana Leung kwa vile alivyokabiliana na hali Hong Kong na pia kup[ongeza polisi kwa namna wanavyokabili maandamano ya maelfu ya watu mjini humo.
Wengi wamekerwa na tamko la China kuwa lazima wanasiasa wenye nia ya kuwania nafasi mjini Hong Kong lazima wakaguliwe na serikali ya China kwa sababu ya uchaguzi utakaofanyika mwaka 2017.
China imeunga mkono polisi kwa namna walivyokabiliana na waandamanaji
Wananchi wa eneo hilo wanasema China haistahili kuingilia siasa zake na wataendelea kuandamana hadi kiongozi wa jimbo hilo atakapoondoka mamlakani.
Serikali imetyaka waandamanaji hao kusitisha maandamano yao ikilaani ghasia na vurugu

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com