Vyombo vya habari vimeripoti kuwa
Wascoti waliokuwa wakipinga uhuru na kujitawala kwa eneo hilo kutoka
Muungano wa Ufalme wa Uingereza wameshinda kwa asilimia 55.42 ya kura
katika kura ya maoni iliyopigwa siku ya Alkhamisi. Watu karibu milioni
4.29 ambao ni asilimia 97 ya jamii ya watu wa Scotland walikuwa
wamejiandikisha kushiriki katika kura hiyo ya maoni iliyolenga kuainisha
mustakbali wa Muungano
wa Ufalme wa Uingereza uliodumu kwa miaka 307.
Mara tu baada ya kutangazwa matokeo ya awali, Alex Salmond, Waziri wa
Kwanza wa Scotland na ambaye pia ni kiongozi wa mrengo wa wanaopigania
uhuru wa eneo hilo kutoka muungano wa Uingereza alikubali kushindwa
katika kura hiyo ya maoni na wakati huohuo kuitaka serikali ya London
itekeleze haraka ahadi ilizotoa kwa eneo hilo kwa kulipatia mamlaka
zaidi ya kujitawala. Salmond Amesema kwa sasa wananchi waliowengi wa
Scotland wameamua eneo hilo lisijitenge na Uingereza na kuwa nchi huru.
Scotland ambayo ina akiba kubwa ya mafuta katika maji yake ya Bahari ya
Kaskazini inaunda Muungano wa Ufalme Uingereza pamoja na maeneo mengine
ya England, Wales na Ireland Kaskazini. Baada ya kutangazwa matokeo ya
kura ya maoni kwa hivi sasa inaonekana kuwa mvutano uliokuwepo kati ya
waungaji mkono na wapinzani wa kujitenga Scotland na muungano wa
Uingereza umekwisha. Kwa kuzingatia kuwa idadi ya waungaji mkono wa
kujitawala Scotland imeongezeka sana katika miaka ya hivi karibuni,
jambo hilo limewatia wasiwasi mkubwa watawala wa Uingereza na hasa
Waziri Mkuu David Cameron ambaye hivi karibuni alitoa ahadi chungu nzima
za kuwapa mamlaka zaidi Wascoti ili kuwashawishi wasijitenge na
kujitawala wenyewe. Wakati huohuo alizungumza kwa maneno makali na
kuwaonya waungaji mkono wa kujitenga eneo hilo waache kufuatilia suala
hilo la sivyo wakabiliwe na matokeo mabaya.
Licha ya matokeo hayo kuwa kwa maslahi ya wapinzani wa kujitenga Scotland, lakini ni wazi kuwa yamewagawa watu wa eneo hilo katika makundi mawili tofauti yanayokaribiana kiidadi. Kundi la kwanza linaona kuwa linataka kuwa na maisha bora kwa kuendelea kubakia katika muungano wa Uingereza na la pili linataka kufikia ndoto yake ya muda mrefu ya kujitawala na hivyo kuacha mashindano ya muda mrefu ya kihistoria, kijografia, kiutamaduni, kimadhehebu na kisiasa na England. Mashindano hayo yalipata kasi na nguvu zaidi tokea miaka 50 iliyopita. Takriban nusu ya Wascoti hujitambulisha kuwa wao ni Wascoti kwanza kabla ya kufikiria kujitambulisha kuwa ni Waingereza. Kwa kuzingatia kuwa waliotaka uhuru wa Scotland wameshindwa kwa kura chache tu, ni wazi kuwa wanawachukulia wapinzani wao kuwa ndio waliowakosesha fursa ya kihistoria ya kujitawala na kwa hivyo hawataacha kupigania kuthibiti kwa ndoto yao ya kujitawala kwa eneo hilo. Ni wazi kuwa wanaotaka uhuru wa Scotland wanaona kuwa wameshindwa katika kura hii ya maoni kutokana na zaidi ya nusu ya watu wa eneo hilo kuamini ahadi zilizotolewa na serikali ya London.

Licha ya matokeo hayo kuwa kwa maslahi ya wapinzani wa kujitenga Scotland, lakini ni wazi kuwa yamewagawa watu wa eneo hilo katika makundi mawili tofauti yanayokaribiana kiidadi. Kundi la kwanza linaona kuwa linataka kuwa na maisha bora kwa kuendelea kubakia katika muungano wa Uingereza na la pili linataka kufikia ndoto yake ya muda mrefu ya kujitawala na hivyo kuacha mashindano ya muda mrefu ya kihistoria, kijografia, kiutamaduni, kimadhehebu na kisiasa na England. Mashindano hayo yalipata kasi na nguvu zaidi tokea miaka 50 iliyopita. Takriban nusu ya Wascoti hujitambulisha kuwa wao ni Wascoti kwanza kabla ya kufikiria kujitambulisha kuwa ni Waingereza. Kwa kuzingatia kuwa waliotaka uhuru wa Scotland wameshindwa kwa kura chache tu, ni wazi kuwa wanawachukulia wapinzani wao kuwa ndio waliowakosesha fursa ya kihistoria ya kujitawala na kwa hivyo hawataacha kupigania kuthibiti kwa ndoto yao ya kujitawala kwa eneo hilo. Ni wazi kuwa wanaotaka uhuru wa Scotland wanaona kuwa wameshindwa katika kura hii ya maoni kutokana na zaidi ya nusu ya watu wa eneo hilo kuamini ahadi zilizotolewa na serikali ya London.
0 toamaon yako: