Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Sunday, September 21

Mazungumzo ya kitaifa Sudan yaungwa mkono

Posted by mkachu  |  Tagged as: , , ,

Mazungumzo ya kitaifa Sudan yaungwa mkonoMwakilishi maalumu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu nchini Sudan amesema kuwa, taasisi hiyo inaunga mkono mazungumzo ya kitaifa nchini humo. Swalah Halima pia ameyataka makundi yenye kubeba silaha na vyama vya upinzani kujiunga na mazungumzo hayo na serikali, ili kutatua matataizo ya kisiasa ya nchi hiyo. Aidha amesifu mpango huo wa mazungumo ya kitaifa uliobuniwa na Rais Omar al Bashir na kusema kwamba, maafisa wa Khartoum wamepiga hatua chanya kwa ajili ya kuandaa mazingira ya mazungumzo.
 Hayo yanajiri huku ikiripotiwa kuwa idadi kubwa ya waasi wa magharibi mwa Sudan wanatarajiwa kutia saini makubaliano ya amani na serikali. Jaafar Abdulhakim kamanda wa jimbo la Darfur amesema kuwa, idadi kubwa ya wanamgambo wa kundi la waasi wa Harakati ya Ukombozi wa Sudan wamejitenga na kundi hilo na kwamba hivi karibuni watatia saini makubaliano ya amani na serikali ya Khartoum.

Related Posts:

0 toamaon yako:

    Author

    CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

    uislam na maisha yake

    uzayuni

    swahili radio

    uislam na maisha

    mohamed waziri

    Subscribe to our Mailing List

    We'll never share your Email address.
    +255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com