Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Sunday, September 21

Milioni 800 wanakabiliwa na balaa la njaa duniani

Posted by mkachu  |  Tagged as:

Milioni 800 wanakabiliwa na balaa la njaa dunianiShirika la Kilimo na Chakula Duniani FAO limetangaza kuwa, zaidi ya watu milioni 800 wanakabiliwa na balaa la njaa duniani. Taarifa iliyotolewa na shirika hilo la Umoja wa Mataifa inaeleza kuwa, katika kila watu tisa mmoja wao anakabiliwa na balaa la njaa duniani. Shirika la FAO limeeleza kuwa, idadi ya watu waliokumbwa na balaa la njaa katika kipindi cha miaka 10 iliyopita ilipungua kwa karibu watu milioni 100 ikilinganishwa na mwaka 1990 ambapo ilikuwa karibu watu milioni 200. Taarifa hiyo inaeleza kuwa, nchi nyingi za Kiafrika na hasa zilizoko katika eneo la kusini mwa jangwa la Sahara barani humo, zinakabiliwa na balaa hilo. Imeelezwa kuwa, watu milioni 214 wanakabiliwa na balaa la njaa barani Afrika. Shirika la Kilimo na Chakula Duniani limeeleza kuwa, nchini Somalia pekee, zaidi ya watu milioni moja wanakabiliwa na balaa la njaa.

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com