Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Sunday, September 21

Iran na Kenya zasisitiza kuimarisha ushirikiano

Posted by mkachu  |  Tagged as:

http://kiswahili.irib.ir/media/k2/items/cache/89c33f3c22d79695003d2a6c2e295d06_XL.jpgMuhammad Yussuf Haji Mkuu wa Kamisheni ya Usalama wa Taifa na Siasa za Kigeni wa Bunge la Seneti la Kenya amekutana na kufanya mazungumzo na Alauddin Bourujerdi Mkuu wa Kamisheni ya Usalama wa Taifa na Siasa za Kigeni wa Majlis ya Ushauri ya Kiislamu yaani ‘Bunge la Iran’ mjini Tehran na pande hizo mbili kusisitiza juu ya kuimarisha mashirikiano katika nyanja zote na hasa katika masuala ya kibunge, kiuchumi na kibiashara. Akizungumzia vikwazo vya kidhuluma vilivyowekwa na nchi za Magharibi dhidi ya Iran, Bourujerdi amesema kuwa, vikwazo hivyo vilivyowekwa yapata miongo mitatu iliyopita, vimepelekea kuimarika moyo wa kujiamini na kusimama kidete kwa wananchi na taifa la Iran. Akizungumzia kuongezeka vitendo vya kigaidi vinavyotishia amani na usalama duniani, Bourujerdi amesisitiza kwamba Iran inapambana na itaendelea kupambana kwa nguvu zake zote dhidi ya ugaidi, kinyume na Marekani na waitifaki wake ambao ndio wasababishaji wakuu wa kuongezeka vitendo vya ugaidi duniani. Mkuu wa Kamisheni ya Usalama wa Taifa na Siasa za Kigeni wa Bunge la Iran amesema kwamba, Iran iko tayari kuinufaisha Kenya kwa uzoefu wake katika masuala ya usalama. Naye Muhammad Yussuf Haji ameeleza kufurahishwa na ziara yake hapa nchini na kusisitiza kwamba, kuimarishwa mashirikiano katika nyanja zote na Iran, nchi ambayo inahesabiwa kuwa muhimu na yenye taathira kubwa katika eneo la Mashariki ya Kati, ni jambo linalozingatiwa na bunge na serikali ya Kenya. Haji ameongeza kuwa, hali inayoshuhudiwa hivi sasa hapa nchini inathibitisha wazi kwamba, licha ya kuwepo mashinikizo na vikwazo vya Wamagharibi, Iran bado imepiga hatua kubwa katika nyanja mbalimbali ikiwemo ya kujipatia nishati ya nyuklia kwa malengo ya amani.

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com