Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Sunday, September 21

Pande hasimu Yemen zafikia makubaliano ya amani

Posted by mkachu  |  Tagged as:

http://kiswahili.irib.ir/media/k2/items/cache/e4c144d2f2a02bd921d38f941cb8b15a_XL.jpg

Mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Yemen amesema kuwa, makubaliano ya usitishaji mapigano yamefikiwa kati ya serikali na wapiganaji wa Houthi. Jamal Bin Omar ameeleza kuwa, makubaliano hayo ni waraka wa kitaifa utakaoandaa njia ya mabadiliko ya amani, na kuweka msingi wa ushirikiano wa kitaifa na kuimarishwa amani na usalama.  Ameongeza kuwa, matayarisho yamefanywa kwa ajili ya kufanyika hafla ya kusainiwa makubaliano hayo ya usitishaji vita hii leo.
Hayo yamejiri baada ya kujiri mapigano makali kati ya vikosi vya serikali na wapiganaji wa Kishia wa Houth ambao walifanikiwa kuzingira kwa muda makao makuu ya televisheni ya taifa mjini San’aa. Zaidi ya watu 100 wamefariki dunia nchini Yemen toka Alkhamisi kutokana na mapigano hayo.
Wafuasi wa Harakati ya Ansarullah na waungaji mkono wao wamekuwa wakifanya maandamano mjini Sana'a kwa zaidi ya mwezi mmoja sasa wakitaka serikali mpya iundwe.

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com