Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Sunday, September 21

Kufutwa kazi Waziri Mkuu wa Uganda

Posted by mkachu  |  Tagged as:

Rais Yoweri Museveni wa Uganda amemfuta kazi Amama Mbabazi Waziri Mkuu wa nchi hiyo. Rais http://kiswahili.irib.ir/media/k2/items/cache/1e2981095f24bfb808a51272bd3ae448_XL.jpgMuseveni hakutaja sababu iliyomfanya amfute kazi Waziri Mkuu wa Uganda. Msemaji wa serikali ya Uganda amesema kuwa kufutwa kazi Mbabazi ni katika fremu ya marekebisho ya baraza la mawaziri. Pamoja na hayo, weledi wa mambo wanaamini kuwa, Amama Mbabazi huwenda akawa miongoni mwa wapinzani wa Rais Yoweri Museveni katika uchaguzi ujao wa rais hapo mwaka 2016.  Amama Mbabazi ni miongoni mwa waitifaki wa siku nyingi wa Museveni na duru za kisiasa za Afrika zinamuona kama ndiye shakhsia nambari moja katika siasa za Uganda. Mbali na kuwa Waziri Mkuu, Amama Mbabazi alikuwa pia Katibu Mkuu wa chama tawala cha Harakati ya Mapambano ya Kitaifa ya Uganda (NRM). Baada ya Mbabazi kuuzuliwa katika kiti cha Katibu Mkuu wa chama tawala mwezi Machi mwaka huu, weledi wa masuala ya kisiasa waliitaja hatua hiyo kuwa ni ishara ya awali ya kuweko mivutano na hitilafu kati ya Museveni na muitifaki wake wa siku nyingi. Hivi sasa baada ya kufutwa kazi Amama Mbabazi katika kiti cha Waziri Mkuu wa Uganda na nafasi yake kuchukuliwa na Ruhakana Rugunda, aliyekuwa Waziri wa Afya, imebainika wazi kwamba hitilafu zimejitokeza kati ya waitifaki hao wawili wa siku nyingi.
Baadhi ya duru za habari zinasema kuwa muswada wa serikali uliopasishwa bungeni hivi karibuni ni moja ya sababu zilizozusha hitilafu hizo. Wawakilishi wa chama tawala ambao wana viti vingi katika Bunge la Uganda, hivi karibuni walipasisha muswada ambao umemruhusu Yoweri Museveni, kiongozi wa chama tawala, kuwa mgombea pekee wa chama hicho katika uchaguzi ujao. Museveni ambaye yuko madarakani huko Uganda tangu mwaka 1986, iwapo atashinda katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2016, basi ataitawala Uganda kwa zaidi ya miaka 30. Kwa msingi huo, tunaweza kumtaja Museveni kuwa ni mmoja wa viongozi wa siku nyingi katika bara la Afrika ambao hawana nia ya kuondoka madarakani. Wakati huo huo Yoweri Kaguta Museveni amekuwa akiwashinda mahasimu wake katika chaguzi zote za rais wa Uganda kwa kuchaguliwa kwa kura za wananchi, japokuwa vyama vya upinzani vinakituhumu chama tawala kuwa kimekuwa kikifanya udanganyifu na kutokuwa na mpangilio katika upigaji kura.
Kwa vyovyote vile, kuna dhana kuwa kufutwa kazi aliyekuwa Waziri Mkuu wa Uganda Amama Mbabazi ni katika jitihada za kufuta ushindani katika uongozi wa chama tawala katika uchaguzi mkuu ujao wa rais.

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com