Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Sunday, September 21

Mahakama ya Ulaya yafuta vikwazo dhidi ya Benki Kuu ya Iran

Posted by mkachu  |  Tagged as:

http://kiswahili.irib.ir/media/k2/items/cache/9aee7f3ac799de7c5c6b92a4df5153bf_XL.jpgMiaka miwili baada ya Baraza la Ulaya kuanza kutekeleza vikwazo vya kidhalimu dhidi ya Benki Kuu ya Iran, Mahakama ya Umoja wa Ulaya imekata shauri kwamba uamuzi wa mwaka 2012 wa baraza hilo wa kuzuia mali za Benki Kuu ya Iran unapaswa kufutiliwa mbali.
Januari mwaka 2012 Umoja wa Ulaya ulisitisha kununua mafuta ya Iran na ukaiwekea vikwazo Benki Kuu ya Jamhuri ya Kiislamu kwa shabaha ya kuzidisha mashinikizo dhidi ya Tehran na kubana shughuli za kuzalisha nishati ya nyuklia hapa nchini. Baada ya uamuzi huo wa Umoja wa Ulaya mali zote za Benki Kuu ya Iran barani Ulaya zilizuiliwa. Mbali na hayo Jumuiya ya Kimataifa ya Kuhamisha Fedha Baina ya Mabenki kwa kifupi (SWIFT) pia ilisitisha huduma zake kwa mabenki ya Iran.
Vikwazo hivyo vya Umoja wa Ulaya vilifuatia azimio la Baraza la Usalama na wakati huo Baraza la Ulaya lilidai kuwa, miongoni mwa sababu za kuiwekea vikwazo Benki Kuu ya Iran ni msaada wa benki hiyo wa kuifanya Iran ikwepe vikwazo vya kimataifa. Iran kwa upande wake iliwasilisha mashtaka kwenye mahakama za Umoja wa Ulaya na sasa mahakama ya umoja huo imetoa hukumu kwamba, Baraza la Ulaya halikuwasilisha ushahidi wowote wa kuthibitisha madai yake dhidi ya Iran na kwa msingi huo vikwazo hivyo vinapaswa kufutwa.
Awali pia mahakama moja ya Ulaya ilitoa hukumu ikiamuru kufutwa vikwazo vya Umoja wa Ulaya dhidi ya makampuni saba ya Iran. Mahakama ya hUlaya ambayo ni ya pili ya juu zaidi ya Umoja wa Ulaya ilitangaza kuwa, umoja huo umeshindwa kuonesha ushahidi wa kuthibitisha kuwa makampuni hayo yanajihusisha na shughuli za nyuklia za Iran.
Katika msimu wa joto kali wa mwaka uliopita, Mahakama ya Juu ya Uingereza pia iliamuru kufutwa vikwazo vya serikali ya nchi hiyo dhidi ya Benki ya Mellat ya Iran. Mahakama hiyo ilisema vikwazo vya serikali ya Uingereza dhidi ya benki hiyo ya Iran si vya kisheria na vinapingana na kanuni.
Katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita makampuni 14, benki na vyuo vikuu vya Iran vimeondolewa katika orodha ya vikwazo vya Ulaya na Marekani kutokana na juhudi zinazofanywa na serikali ya sasa ya Tehran kwa ajili ya kuondolewa vikwazo vilivyowekwa na nchi hizo. Hukumu ya sasa ya Mahakama ya Umoja wa Ulaya ya kufuta vikwazo vilivyowekwa na nchi za bara hilo dhidi ya Benki Kuu ya Iran japokuwa ni ya mwanzo ya mahakama hiyo na inaweza kukatiwa rufaa, lakini iwapo itapasishwa inaweza kuwa na taathira kubwa nzuri katika mfumo wa fedha na miamala ya kibiashara ya Iran. Kuondolea kwa vikwazo hivyo kutaiwezesha Iran kurejesha nchini mamilioni ya dola za mauzo ya mafuta na bidhaa nyingine kutoka nje kwa ajili ya ustawi wa nchi. Iwapo vikwazo hivyo vya Umoja wa Ulaya vitafutwa, Iran itaweza kupeleka na kupokea fedha kutoka nchi za kanda ya Euro. Vilevile Iran itazidisha kiwango cha biashara zake na nchi za Ulaya, gharama za usafirisha wa fedha zitapungua sana na kasi ya mabadilishano ya kifedha itaongezeka.
Inaonekana kuwa kutolewa hukumu ya Mahakama ya Umoja wa Ulaya katika kipindi cha sasa cha duru mpya ya mazungumzo ya Iran na kundi la 5+1 yanayofanyika kandokando ya mkutano wa kila mwaka wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York, hakukutokea kwa sadfa. Hukumu hiyo inaweza kuwa ujumbe wa nchi za Ulaya kwa Marekani kwamba hazitaki tena kuendeleza vikwazo dhidi ya Iran na kwamba yumkini Marekani ikabakia peke yake katika kudumisha mashinikizo yake dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu.

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com