Rais Hassan Sheikh Mohamud wa Somalia ameitaka jamii ya kimataifa
kuizingatia kimisaada nchi yake kutokana na hali mbaya inayolikabili
taifa hilo. Rais Mohamud ameyasema hayo katika hotuba aliyoitoa mbele ya
kikao cha 69 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York, na
kuongeza kuwa, hali ya kibinaadamu nchini mwake ni mbaya sana. Alisema
kuwa ili kukabiliana na hali hiyo serikali ya Mogadishu inahitajia
msaada wa kifedha wa takriban dola nusu bilioni. Alisema kuwa, watu
milioni tatu na laki mbili wanahitajia msaada wa haraka nchini Somalia
huku karibu watu milioni moja wengine wakikabiliwa na mgogoro wa
chakula. Rais wa Somalia ameongeza kuwa, hadi sasa nchi yake bado
imepokea nusu pekee ya misaada ya kimataifa iliyoahidiwa. Aidha
amesisitizia umuhimu wa maendeleo ya kuimarisha usalama nchini humo na
kusema kuwa, hii leo Somalia si nchi inayoweza kushindwa tena na
ash-Shabab. Itakumbukwa kuwa, mwaka 2011 Somalia ilikumbwa na baa la
njaa lililosababishwa na ukame, na kupelekea idadi kubwa ya watu
kupoteza maisha.
IQRA FM RADIO
Friday, September 26
Browse: Home
» Habari za kitaifa na kimataifa
» Rais H. Mohamud: Jamii ya kimataifa iisaidie Somalia
Rais H. Mohamud: Jamii ya kimataifa iisaidie Somalia
Posted by mkachu |  Tagged as: Habari za kitaifa na kimataifa
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Andika Maoni
add
LEO KATIKA HISTORIA
TANGAZANASI
kwama Matangazo wasiliana nasi kupitia anuani zifuataz
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
ZILIZO SOMWA ZAIDI
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa ni dua za baada ya nyakati mbalimbali za sala. Tunamuomba Mwenyezi Mung...
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa chini ni dua 25 za Qur'ani Tukufu tulizozinukuu kutoka katika...
-
RATIBA YA VIPINDI KWA JUMA ZIMA RATIBA - JUMATATU MUDA KIPINDI MUHUSIKA 06:30-07:00 M...
-
Rais Bashar al-Assad wa Syria amesema kuwa, kuna udharura wa kuweko vita vya kimataifa dhidi ya magaidi. Rais Assad amesisitiza kwamba, kwa...
MITANDAO YA KIJAMII
TAFUTA HABARI ZILIZO SOMWA NYUMA
Powered by Blogger.
Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...
0 toamaon yako: