Leo ni Jumamosi tarehe Pili Mfunguo tatu Dhil-Hijja 1435 Hijria sawa na tarehe 27 Septemba 2014 Miladia.
Siku kama ya leo miaka 33 iliyopita
wapiganaji shujaa wa Iran walifanikiwa kuvunja mzingiro wa mji wa Abadan
katika operesheni ya haraka na iliyokuwa imeratibiwa vyema dhidi ya
ngome za jeshi la Saddam Hussein. Operesheni hiyo ilitekelezwa na
wapiganaji wa Iran kufuatia agizo la kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu
Imam Khomeini Mwenyezi Mungu amrehemu. Mji wa Abadan ulikuwa umezingirwa
na wanajeshi wa Iraq kwa karibu mwaka mmoja tangu kuanza vita vya
kulazimishwa vya utawala wa dikteta Saddam dhidi ya Iran. ***
Katika siku kama ya leo miaka 65
iliyopita, mji wenye jamii kubwa ya watu wa Beijing ulichaguliwa rasmi
kuwa mji mkuu wa Uchina. Mji wa kihistoria wa Beijing unapatikana
mashariki kwa nchi hiyo na unahesabiwa kuwa moja ya vituo vikubwa vya
kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni vya China. Beijing ulichaguliwa kuwa
mji mkuu wa China baada ya Mao Tse-tung kuchukua madaraka ya nchi na
kiongozi wa wakati huo wa China Chiang Kai-shek akakimbilia Taiwan. ***
Miaka 73 iliyopita katika siku kama ya leo, jeshi la Ujerumani ya Kinazi lilipata ushindi mkubwa wakati lilipokuwa likisonga mbele kuelekea huko Urusi ya zamani katika vita vilivyokuwa vimeanza mwezi Juni mwaka 1941. Wanajeshi wa Urusi ya zamani walikabiliwa na mashambulizi ya pande zote ya vikosi vya Ujerumani wakati wakiwa wamechoka na kuishiwa zana za kivita. Mapigano kati ya pande mbili hizo yalipelekea kutekwa nyara wanajeshi wa Urusi ya zamani zaidi ya laki sita na kuharibiwa karibu vifaru 1200 na mizinga 5400 ya nchi hiyo. ***
Miaka 73 iliyopita katika siku kama ya leo, jeshi la Ujerumani ya Kinazi lilipata ushindi mkubwa wakati lilipokuwa likisonga mbele kuelekea huko Urusi ya zamani katika vita vilivyokuwa vimeanza mwezi Juni mwaka 1941. Wanajeshi wa Urusi ya zamani walikabiliwa na mashambulizi ya pande zote ya vikosi vya Ujerumani wakati wakiwa wamechoka na kuishiwa zana za kivita. Mapigano kati ya pande mbili hizo yalipelekea kutekwa nyara wanajeshi wa Urusi ya zamani zaidi ya laki sita na kuharibiwa karibu vifaru 1200 na mizinga 5400 ya nchi hiyo. ***
Na miaka 18 iliyopita katika siku kama
ya leo, kundi la Taliban lilivamia na kutwaa mji mkuu wa Afghanistan,
Kabul. Kundi hilo liliasisiwa mwaka 1994 na likateka hatua kwa hatua
maeneo ya kusini na magharibi mwa Afghanistan kwa himaya ya Marekani,
misaada ya kisiasa na kijeshi ya Pakistan pamoja na misaada ya kifedha
ya Saudi Arabia. Jeshi la serikali ya Afghanistan lililokuwa likiongozwa
na Ahmad Shah Mas'ud liliondoka mjini Kabul siku moja kabla ya Taliban
kuuteka mji huo. Baada ya kuingia Kabul, kundi la Taliban lilianza
kutekeleza sheria kali na zinazoshabihiana na zile za karne za kati
dhidi ya wananchi.

Facebook
Twitter
RSS
0 toamaon yako: