Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Friday, September 26

Kiongozi wa Boko Haram atiwa mbaroni Cameroon

Posted by mkachu  |  Tagged as:

Kiongozi wa Boko Haram atiwa mbaroni CameroonJeshi la Cameroon limetangaza habari ya kutiwa mbaroni kiongozi mwengine mwandamizi wa kundi la Boko Haram, nchini humo. Jeshi la Cameroon limemtaja kiongozi huyo kuwa ni Ababakar Ali maarufu kwa jina la Moustapha Oumar na kwamba alitiwa mbaroni kaskazini mwa nchi hiyo akiwa na walinzi wake wawili waliofahamika kwa majina ya Muhamed Ali na Issiaka Gare. Viongozi wa usalama nchini Cameroon wamesema kuwa, Ababakar Ali alikuwa akijishughulisha na ukusanyaji wa ripoti kwa ajili ya kundi hilo kwa lengo la kufanya mashambulizi na kusimamia shughuli za wanachama wa kundi hilo lenye uelewa potofu kuhusiana na mafundisho sahihi ya dini ya Kiislamu. Aidha jeshi hilo limefanikiwa kunasa maficho ya silaha katika operesheni za kumtia mbaroni kiongozi huyo wa Boko Haram. Ababakar Ali ni mmoja wa viongozi wa kundi hilo ambaye pia alikuwa amekodi jengo na kulitumia kama maficho ya silaha za kundi hilo. Inaelezwa kuwa katika nyumba hiyo kumekutwa silaha mbalimbali zikiwemo bunduki na makombora na kwamba jeshi la Cameroon limefaniwa kumtia mbaroni kiongozi huyo kwa ushirikiano wa wananchi waliotilia shaka mienendo ya mtu huyo.

 

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com