Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Friday, September 26

Rais Condé alaani jinai za Israel Ukanda wa Gaza

Posted by mkachu  |  Tagged as:

Rais Condé alaani jinai za Israel Ukanda wa GazaRais Alpha Condé wa Guinea amesema kuwa, kuheshimiwa mipaka ya mwaka 1967 ndio njia pekee ya kuweza kufikiwa usalama katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu. Rais Condé ameyasema hayo katika kikao cha 69 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York, ambapo pamoja na mambo mengine, amesisitiza juu ya uungaji mkono wa nchi yake kwa taifa la Palestina na kulaani vikali jinai za utawala wa Kizayuni dhidi ya Ukanda wa Ghaza huku akiitaka Tel Aviv kuheshimu sheria za kimataifa. Vile vile Rais huyo wa Guinea ameashiria ongezeko la umasikini na uharibifu wa mazingira unaofanywa na wanadamu na kutaka kuwekwa mikakati madhubuti ya kukabiliana na matatizo hayo. Aidha ameashiria mgogoro wa afya nchini Sierra Leone, Liberia na Guinea Conakry na kutaka kukabiliana kwa nguvu zote na janga hilo ambalo linazidi kushika kasi siku hadi siku katika nchi za magharibi mwa Afrika. Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), karibu watu 3,000 wamekwishapoteza maisha tangu mwezi Machi mwaka huu kulipoibuka ugonjwa huo hatari wa Ebola huko magharibi mwa Afrika.

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com