Mfuko wa Fedha wa Kimataifa (IMF)
umetangaza kutengwa kiasi cha dola milioni 130 kwa ajili ya kukabiliana
na maambukizi ya ugonjwa wa Ebola. Ripoti iliyotolewa na IMF imesisitiza
kuwa kiwango hicho cha fedha kitakabidhiwa kwa nchi za magharibi mwa
Afrika zikiwemo Guinea Conakry, Liberia na Sierra Leone ambazo
zimeathiwa zaidi na ugonjwa huo. Aidha ripoti hiyo imefafanua kuwa
msaada huo wa fedha umetengwa kufuatia ombi la nchi hizo juu ya
kukabiliana na janga hilo. Siku ya Alkhamisi nchi za Ujerumani, Canada,
Marekani, Ufaransa, Italia, Japan na Uingereza ambazo ni wanachama wa
kundi la G7, maambukizi ya ugonjwa huo yanapaswa kudhibitiwa kwa njia
yoyote ile, lakini zikasisitiza pia juu ya kutotengwa nchi
zilizoathiriwa na tatizo hilo. Viongozi wa nchi hizo waliyasema hayo
kando na kikao cha 69 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York.
Ugonjwa wa Ebola uliibuka mwishoni mwa mwaka jana nchini Guinea Conakry
na kuenea kwa haraka katika nchi nyingine jirani kama Liberia, Sierra
Leone, Nigeria na Senegal.
IQRA FM RADIO
Friday, September 26
IMF: Dola milioni 130 zimetengwa kuikabili Ebola
Posted by mkachu |  Tagged as: Habari za kitaifa na kimataifa
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Andika Maoni
add
LEO KATIKA HISTORIA
TANGAZANASI
kwama Matangazo wasiliana nasi kupitia anuani zifuataz
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
ZILIZO SOMWA ZAIDI
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa ni dua za baada ya nyakati mbalimbali za sala. Tunamuomba Mwenyezi Mung...
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa chini ni dua 25 za Qur'ani Tukufu tulizozinukuu kutoka katika...
-
RATIBA YA VIPINDI KWA JUMA ZIMA RATIBA - JUMATATU MUDA KIPINDI MUHUSIKA 06:30-07:00 M...
-
Rais Bashar al-Assad wa Syria amesema kuwa, kuna udharura wa kuweko vita vya kimataifa dhidi ya magaidi. Rais Assad amesisitiza kwamba, kwa...
MITANDAO YA KIJAMII
TAFUTA HABARI ZILIZO SOMWA NYUMA
Powered by Blogger.
Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...
0 toamaon yako: