Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Friday, September 26

Mashambulio ya US dhidi ya Daesh ni ya kimaonyesho

Posted by mkachu  |  Tagged as:

Mashambulio ya US dhidi ya Daesh ni ya kimaonyeshoRais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, mashambulizi ya anga ya Marekani dhidi ya kundi la Daesh ni ya kimaonyesho. Rais Rouhani amesema kuwa, mashambulizi hayo hayawezi kukabiliana wala kuliangamiza kundi hilo ambalo linahama kutoka sehemu moja kwenda nyingine. Rais Rouhani alisema hayo jana katika mahojiano na kanali ya televisheni ya Marekani ya CNN, na kusisitiza kuwa, mashambulizi ya Marekani dhidi ya kundi hilo, ni vita vya kisaikolojia na wala si operesheni za kijeshi kama inavyodaiwa na Washington. Rais Hassan Rouhani amesema, mashambulizi hayo ni hadaa kwa ulimwengu. Kwengineko Rais Rouhani ameashiria mazungumzo ya nyuklia kwa kusema kuwa, kufikiwa makubaliano ya muda mfupi, ni ishara kwamba mazungumzo yamefanikiwa. Amesema kuwa kila upande wa mazungumzo unaamini kuwa, mazungumzo ndio njia pekee ya utatuzi wa kadhia ya nyuklia na si vinginevyo. Hii ikiwa na maana kwamba, vikwazo na vitisho ni mambo yasiyo na nafasi yoyote ile.

 

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com