Naibu Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Iran amesema kuwa, Tehran ina
shaka na nia ya Marekani ya kutaka kupambana na ugaidi. Akizungumza na
ujumbe wa maseneta kutoka nchini Kenya ulioko nchini, Hussein Amir
Abdulahiyan amesema kuwa, mara baada ya kuanza mgogoro wa Syria, Iran
ilizitahadharisha nchi za Magharibi juu ya matokeo mabaya na hatari ya
kuyaunga mkono makundi ya kigaidi. Abdulahiyan ameongeza kuwa, baada ya
kupita muongo mmoja makundi yanayofungamana na al Qaeda yamekuwa na
uzoefu mkubwa katika kutekeleza operesheni zao za kigaidi katika nchi za
Afghanistan na Iraq. Naibu Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Iran
amesema kuwa, uhusiano wa Tehran na Nairobi uko katika kiwango kizuri,
na kusisitiza kwamba nafasi ya mabunge na hasa Kamisheni ya Usalama wa
Taifa na Sera za Kigeni ina nafasi muhimu mno. Kwenye mazungumzo hayo,
Muhammad Yussuf Haji, Mkuu wa Kamisheni ya Usalama wa Taifa na Sera za
Kigeni katika Bunge la Seneti la Kenya ameelezea azma ya serikali ya
nchi yake ya kuimarisha mashirikiano na Iran na kusisitiza kwamba
Nairobi ina taarifa za kutosha kuhusu hatua kubwa za maendeleo
zilizopigwa na Iran katika nyanja za elimu na teknolojia. Haji ameongeza
kuwa, Kenya inataka mashirikiano ya pande mbili katika nyanja
mbalimbali yaimarishwe zaidi.
IQRA FM RADIO
Tuesday, September 23
Maseneta wa Kenya wakutana na Naibu Waziri wa Iran
Posted by mkachu |  Tagged as: Habari za kitaifa na kimataifa
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Andika Maoni
add
LEO KATIKA HISTORIA
TANGAZANASI
kwama Matangazo wasiliana nasi kupitia anuani zifuataz
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
ZILIZO SOMWA ZAIDI
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa ni dua za baada ya nyakati mbalimbali za sala. Tunamuomba Mwenyezi Mung...
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa chini ni dua 25 za Qur'ani Tukufu tulizozinukuu kutoka katika...
-
RATIBA YA VIPINDI KWA JUMA ZIMA RATIBA - JUMATATU MUDA KIPINDI MUHUSIKA 06:30-07:00 M...
-
Sura ya Al Furqan, aya ya 41-44 (Darsa ya 628) Wasikilizaji wapenzi wa Darsa ya Qur'ani, Assalamu Alaykum Warahmatullahi Wa...
MITANDAO YA KIJAMII
TAFUTA HABARI ZILIZO SOMWA NYUMA
Powered by Blogger.
Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...
0 toamaon yako: