Kundi la watu wenye misimamo ya chuki dhidi ya dini tukufu ya Kiislamu
nchini Ufaransa wameuvunjia heshima Msikiti katika eneo la mashariki mwa
nchi hiyo. Gazeti la Le Figaro linalochapishwa nchini Ufaransa
limeandika kuwa, mfanyakazi wa msikiti ulioko katika eneo la Pontarlier
mashariki mwa Ufaransa, jana aliushuhudia mzoga wa nguruwe uliotupwa
kwenye mlango wa kuingilia msikitini. Taasisi kadhaa za Kiislamu nchini
Ufaransa zimetoa tamko la kulaani vikali kitendo hicho, kinachokinzana
na uhuru wa kuabudu. Polisi ya Ufaransa imeshaanza uchunguzi kuhusiana
na kitendo hicho kinachoonyesha wazi kuwepo chuki dhidi ya dini ya
Kiislamu nchini humo. Kiongozi wa serikali katika eneo hilo amelaani
kitendo hicho na kusisitiza kwamba, serikali ya Paris itaendeleza juhudi
za kuwasaka na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria wahusika wote wa
kitendo hicho. Naye mmoja kati ya viongozi wa Baraza la Waislamu wa
Ufaransa CFCM amesema kuwa, tokea yaliposhadidi machafuko katika eneo la
Mashariki ya Kati, vitendo vya chuki na uadui dhidi ya dini ya Kiislamu
vimeongezeka, katika hali ambayo Waislamu wanataka kuishi na wafuasi wa
dini nyingine nchini humo kwa amani.
IQRA FM RADIO
Tuesday, September 23
Maadui wauvunjia heshima Msikiti nchini Ufaransa
Posted by mkachu |  Tagged as: Habari za kitaifa na kimataifa
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Andika Maoni
add
LEO KATIKA HISTORIA
TANGAZANASI
kwama Matangazo wasiliana nasi kupitia anuani zifuataz
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
ZILIZO SOMWA ZAIDI
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa ni dua za baada ya nyakati mbalimbali za sala. Tunamuomba Mwenyezi Mung...
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa chini ni dua 25 za Qur'ani Tukufu tulizozinukuu kutoka katika...
-
RATIBA YA VIPINDI KWA JUMA ZIMA RATIBA - JUMATATU MUDA KIPINDI MUHUSIKA 06:30-07:00 M...
-
Sura ya Al Furqan, aya ya 41-44 (Darsa ya 628) Wasikilizaji wapenzi wa Darsa ya Qur'ani, Assalamu Alaykum Warahmatullahi Wa...
MITANDAO YA KIJAMII
TAFUTA HABARI ZILIZO SOMWA NYUMA
Powered by Blogger.
Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...
0 toamaon yako: