Rais Ibrahim Boubacar Keita wa Mali ametoa wito wa kupatikana maridhiano
ya kitaifa katika nchi hiyo ya magharibi mwa Afrika inayokabiliwa na
mgogoro wa kisiasa na kiusalama. Rais Keita amesisitiza juu ya udharura
wa kupatikana maridhiano ya kitaifa katika maeneo yote ya nchi hiyo.
Rais wa Mali ameashiria mazungumzo ya amani yanayoendelea huko Algeria
kati ya ujumbe wa serikali ya Bamako na wapinzani na kusisitiza kwamba,
bila shaka hata hao wanaoshiriki katika mazungumzo hayo wanataka
kufikiwa maridhiano ya kitiafa katika nchi yao. Duru ya pili ya
mazungumzo ya amani kati ya serikali ya Mali na makundi yanayobeba
silaha ya kaskazini mwa nchi hiyo ilianza tarehe Mosi mwezi huu katika
mji mkuu wa Algeria, Algiers. Awamu ya kwanza ya mazungumzo hayo
ilifanyika tarehe 4 Julai katika mji huo huo ambapo pande mbili zilitia
saini ramani ya njia ya mazungumzo kati yao. Serikali ya Mali imekuwa
ikikabiliwa na mgogoro wa kisiasa tangu Januari mwaka 2012 baada ya
makundi yenye silaha kuanzisha mashambulio katika maeneo ya kaskazini
mwa nchi hiyo.
IQRA FM RADIO
Tuesday, September 23
Browse: Home
» Habari za kitaifa na kimataifa
» Keita asisitizia kupatikana maridhiano ya kitaifa Mali
Keita asisitizia kupatikana maridhiano ya kitaifa Mali
Posted by mkachu | Tagged as: Habari za kitaifa na kimataifa
Related Posts:
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Andika Maoni
add
LEO KATIKA HISTORIA
TANGAZANASI
kwama Matangazo wasiliana nasi kupitia anuani zifuataz
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
ZILIZO SOMWA ZAIDI
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa ni dua za baada ya nyakati mbalimbali za sala. Tunamuomba Mwenyezi Mung...
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa chini ni dua 25 za Qur'ani Tukufu tulizozinukuu kutoka katika...
-
RATIBA YA VIPINDI KWA JUMA ZIMA RATIBA - JUMATATU MUDA KIPINDI MUHUSIKA 06:30-07:00 M...
-
Sura ya Al Furqan, aya ya 41-44 (Darsa ya 628) Wasikilizaji wapenzi wa Darsa ya Qur'ani, Assalamu Alaykum Warahmatullahi Wa...
MITANDAO YA KIJAMII
TAFUTA HABARI ZILIZO SOMWA NYUMA
Powered by Blogger.
Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...
0 toamaon yako: