anjari na kuendelea maandamano ya
wananchi wanaotaka haki zao za kimsingi, hivi sasa Saudia inakabiliwa
pia na ongezeko la fikra za makundi ya kufurutu ada nchini humo. Kuanzia
Ijumaa iliyopita eneo la Qatwif, mashariki mwa nchi hiyo, limekuwa
likishuhudia maandamano ya wananchi dhidi ya utawala wa kifalme wa nchi
hiyo. Katika maandamano hayo, waandamanaji wanasisitizia juu ya
kuachiliwa huru wafungwa wa kisiasa na kuhitimishwa ukandamizaji na
mashinikizo dhidi ya raia. Hata hivyo duru za habari nchini humo
zinaarifu kuwa, katika kujaribu kuzima maandamano hayo, askari wa
Aal-Saud wamekuwa wakishambulia Swaandamanaji kwa risasi na mabomu ya
kutoa machoni, na kupelekea kujeruhiwa makumi ya waandamanaji huku
wengine wakitiwa mbaroni. Aidha askari hao wa Saudia, wamemtia mbaroni
Basim al-Qudayhi, kijana aliyejeruhiwa vibaya katika maandamano ya siku
za nyuma na ambaye alikuwa bado anaendelea kupata matibabu hospitalini
kwa lengo la kuokoa maisha yake. Wizara ya Mambo ya Ndani ya Saudia
sanjari na kuthibitisha kutiwa mbaroni al-Qudayhi, imetangaza kuwa
kijana huyo alitiwa mbaroni kwa tuhuma za kuhusika eti na mashambulizi
ya silaha dhidi ya maafisa usalama, kutishia maisha ya raia n
a kutoa
mafunzo ya kijeshi kwa watoto wadogo wa nchi hiyo, tuhuma ambazo
zimetajwa na wapinzani kuwa ni za kubambikiziwa al-Qudayhi na ambazo
hadi sasa hazijathibitishwa na pande zozote huru. Hii ni katika hali
ambayo wakazi wengi wa mkoa wa al-Sharqiyyah, hapo jana asubuhi pia
walifanya maandamano ya amani yaliyoitishwa na Muungano wa Uhuru na
Uadilifu chini ya kaulimbiu ya 'Lazima Kuvunjwa Mzingiro', maandamano
ambayo pia yalikabiliwa na hujuma ya askari usalama wa Saudia. Hapo jana
mtandao wa habari wa al-Ahd wa Saudia pia uliandika kuwa, kuanzia
asubuhi ya jana Jumamosi, mji wa Qatwif ulizingirwa kikamilifu na askari
wa utawala wa Aal-Saud sanjari na kuwekwa vituo vya ukaguzi vya kutoka
na kuingia katika mji huo. Mbali na hayo, nchini Saudia kumeripotiwa
habari za ongezeko la fikra za kufurutu ada za Kidaesh katika maeneo
tofauti ya nchi hiyo suala ambalo linatajwa kuwatia khofu watawala wa
Riyadh. Kuhusu hilo, maandishi yafautayo, "Daesh imo katika mioyo yetu,"
yalipatikana yameandikwa katika moja ya milango ya shule za wasichana
iliyoko katika mji wa Al Khurma, kaskazini mashariki mwa mkoa wa Taif,
maandishi ambayo yamewaogofya sana viongozi wa Saudia. Kwa mujibu wa
duru za habari, maafisa usalama katika mkoa huo wameanzisha upelelezi wa
kugundua mwandishi wa maneno hayo. Inaelezwa kuwa, uharibifu wa mali za
umma na kadhalika kuenea kwa fikra za kufurutu ada, ni sababu mbili
muhimu zilizopelekea viongozi wa Saudia kuanzisha uchunguzi wa mwandishi
wa maneno hayo. Ni vyema kufahamika hapa kuwa, wasiwasi wa viongozi wa
utawala wa kifalme nchini Saudia juu ya ongezeko la fikra za kufurutu
ada hususan fikra za Kidaesh, unakuja katika hali ambayo kwa kipindi cha
miaka ya hivi karibuni Saudia imekuwa moja ya waungaji mkono wakuu wa
makundi ya kigaidi likiwemo kundi hili la kitakfiri na kigaidi
linalojiita eti Dola la Kiislamu nchini Iraq na Sham 'Daesh'. Hivi sasa
sanjari na utawala huo kufanya njama za kuzima au kupunguza wimbi la
maandamano dhidi yake, unapaswa pia kukabiliana au kupunguza fikra za
kitakfiri na tishio la makundi ya kigaidi hususan lile la Daesh nchini
humo.
IQRA FM RADIO
Sunday, September 28
Browse: Home
» Uislamu
» Kuendelea maandamano sambamba na ongezeko la fikra za kufurutu ada nchini Saudia
Kuendelea maandamano sambamba na ongezeko la fikra za kufurutu ada nchini Saudia
Posted by mkachu |  Tagged as: Habari za kitaifa na kimataifa, Uislamu
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Andika Maoni
add
LEO KATIKA HISTORIA
TANGAZANASI
kwama Matangazo wasiliana nasi kupitia anuani zifuataz
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
Email:
iqrafmradio@gmail.cm
contact us:
0752925259
0762118805
infohttp:iqrafmradio.blogspot.com
uimara wa redio iqra upo mikononi mwako
>>Wote mnakalibishwa.....................................
ZILIZO SOMWA ZAIDI
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa ni dua za baada ya nyakati mbalimbali za sala. Tunamuomba Mwenyezi Mung...
-
Mwenyezi Mungu anasema: Niombeni nitakupeni. Zifuatazo hapa chini ni dua 25 za Qur'ani Tukufu tulizozinukuu kutoka katika...
-
RATIBA YA VIPINDI KWA JUMA ZIMA RATIBA - JUMATATU MUDA KIPINDI MUHUSIKA 06:30-07:00 M...
-
Sura ya Al Furqan, aya ya 41-44 (Darsa ya 628) Wasikilizaji wapenzi wa Darsa ya Qur'ani, Assalamu Alaykum Warahmatullahi Wa...
MITANDAO YA KIJAMII
TAFUTA HABARI ZILIZO SOMWA NYUMA
Powered by Blogger.
Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...
0 toamaon yako: