Tanzania swahili radio

IQRA FM RADIO

IQRA FM RADIO
IQRA FM RADIO ELIMU NA MATENDO UIMARA WA RADIO IQRA UPO MIKONOMI MWAKO CHANGIA RADIO IQRA KWA MPESA 0762118805TIGO PESA 0658118804

Sunday, September 28

Jumapili, 28 Septemba 2014 20:01 Wanachuo wapinga safari Sisi Chuo Kikuu cha Cairo

Posted by mkachu  |  Tagged as: ,

Wanachuo wapinga safari Sisi Chuo Kikuu cha CairoKundi la wanafunzi wa Vyuo Vikuu vya Misri leo Jumapili limefanya maandamano katika meidani ya Tahrir wakipinga safari ya leo alasiri ya Rais Abdul Fatah al Sisi wa nchi hiyo katika Chuo Kikuu cha Cairo. Makumi ya wanachuo ambao ni wanachama wa Harakati ya Wanachuo wanaopinga mapinduzi ya kijeshi wameshiriki kwenye maandamano hayo katika meidani ya Tahrir huko Cairo na kupiga nara dhidi ya Rais wa Misri na utawala ulioko madarakani. Wanachuo hao wametangaza kuwa hii ni hatua yao ya kwanza katika kupinga safari ya Rais wa Misri katika Chuo Kikuu cha Cairo. Hii ni katika hali ambayo, mw aka jana Vyuo Vikuu vya nchini Misri karibu kila siku vilikuwa vikishuhudia maandamano makubwa ya wanachuo wafuasi wa Mohamed Morsi Rais wa zamani wa nchi hiyo aliyepinduliwa na jeshi, maandamano ambayo wakati mwingine yalikuwa yakisababisha ghasia na machafuko na kupelekea wanachuo kadhaa kuuawa na kujeruhiwa na makumi ya wengine kutiwa nguvuni. Aidha wanafunzi wengine wa Vyuo Vikuu nchini Misri walifukuzwa chuo kutokana na kushiriki kwao katika maandamano.

0 toamaon yako:

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

uislam na maisha yake

uzayuni

swahili radio

uislam na maisha

mohamed waziri

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com